• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yaombwa kuanzisha sera ya Taifa ya Wajane

Imewekwa tarehe: June 23rd, 2019

WAJANE nchini wameiomba Serikali kuwapa kuandaa sera ya Taifa itakayowatambua kama kundi maalum katika jamii ili haki zao ziweze kulindwa.

Wametoa kauli hiyo imetolewa wakati wa maandamano yaliyohitimisha maadhimisho ya siku ya wajane duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Nyerere Jijini Dodoma leo.

Mmoja wa Wajane hao Nyabumera alisema “tunaiomba Serikali itoe ushirikiano na kusaidia uanzishaji wa Sera ya taifa ya wajane itakayowatambua wajane kama kundi maalum katika jamii” alisema.

Alisema uanzishwa kwa sera ya Taifa kwa ajili ya wajane kutasaidia kutoa msukumo kwa jamii juu ya haki na madhila wanayopitia wajane na kwamba kundi hilo limekuwa likidhulumiwa mali pindi wenzi wao wanapofariki.

Nyabumera alishauri vifo vya wanaume vitambuliwe kuwa vinatokana na mapenzi ya Mungu kama vilivyo vifo vya wanawake. “Pendekezo langu vifo vya wanaume navyo vitambuliwe kuwa vinatokana na mapenzi ya Mungu kama vilivyo vifo vya wanawake na siyo kurogwa, jambo hilo ndilo linalosababisha wajane tunakosa haki zetu baada ya kufiwa na waume zetu” alisema Nyabumera huku akishauri jamii ijenge utamaduni wa kuandika wosia ili kuwasaidia wenzi wao kuwa salama na kumiliki mali walizochuma pamoja na waume zao.

Nae mkazi wa Jijini Dodoma, Lusy Sanga alisema kuwa wajane wamekuwa wakipitia mateso makubwa na kuangukia katika wimbi la umasikini. “Baada ya mume wangu kufariki, ndugu wa mume walichukua mali zote na kuuza nyumba” alisema Sanga na kufafanua kuwa baada ya tukio hilo hali ya maisha ilibadilika na kuwa ngumu jambo lililomlazimisha kufanya kazi usiku na mchana ili kuweza kuwahudumia watoto wake saba.

Akiongelea changamoto zinazowakabili wanawake wajane, mkazi wa Mwanza Antonia Zacharia aliyeshiriki maadhimisho hayo alisema kuwa, wanakabiliwa na changamoto nyingi zinazodidimiza juhudi zao za kujiletea maendeleo. 

Alisema miongoni mwa changamoto hizo ni kutengwa na ndugu wa mume baada ya mume kufariki na wajane kunyanyaswa na kunyang’anywa mali zote na ndugu wa mume wakidai kuwa ni mali zao na pale wanapolazimika kudai mali hizo hutakiwa kutoa rushwa na ngono.

Maadhimisho ya siku ya wajane duniani yamefanyika kitaifa jijini Dodoma yakiwa ni maadhimisho ya kwanza kufanyika kitaifa yakiongozwa na kaulimbiu isemayo “Wezesha mafunzo ya ujuzi kwa wajane: Changia kufikia malengo ya maendeleo endelevu”, ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Faustine Dugulile.

Maandamano ya wajane wakielekea uwanja wa Nyerere Square kuhitimisha Siku ya Wajane Duniani.

Wajane wakiandamana kitaifa kusherehekea siku ya wajane duniani

Wanawake wajane wakipaza sauti kukemea changamoto wanazokutana nazo kwenye maisha ya ujane


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.