• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yapongeza wanaolea yatima

Imewekwa tarehe: March 12th, 2019

SERIKALI imewapongeza watawa wanaosimamia watoto yatima wa kituo cha Nyumba ya Matumaini kilichopo Kata ya Miyuji Halmashauri ya jiji la Dodoma kwa kazi ya kulea watoto hao.

Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Madhimisho ya siku ya Wanawake katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Hildagrace Makwinya hivi karibuni katika kituo hicho.

Makwinya alisema “napenda kuwapongeza sana watawa wanaolea watoto hawa katika kituo hiki cha nyumba ya Matumaini, pongezi kwa kazi ya ulezi mliyonayo, hakika ninyi ni kina mama na kina baba kwa hawa watoto kazi mnayofanya ni nzuri na kubwa”, aliongeza.

Akiongelea changamoto inayowakabili watoto wa kituo hicho ya kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa alisema, serikali italishughulikia suala hilo.

“Nimepokea tatizo la watoto wengi katika kituo hiki cha nyumba ya Matumaini kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa jambo linalosababisha watoto hawa wakose baadhi ya huduma muhimu. Bahati nzuri wizara yetu ya Sheria na Katiba ndiyo inahusika na usajili huo” alisema Makwinya.

“Nitawasiliana na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) ili kuhakikisha watoto hawa wanasajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa kwa mujibu wa taratibu” aliongeza.

Naye Mkuu  wa idara ya Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya alisema kuwa, jukumu la kulea watoto ni zito na linalohitaji uwajibikaji wa pamoja.

“Hakika mnafanya kazi ya Mungu, napenda kuwatia moyo japo kuna changamoto ila malipo yenu ya uhakika ni mbinguni…Serikali ipo pamoja nanyi na nichukue nafasi hii kuwakaribisha katika katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji mnapokuwa na changamoto zinazohitaji utatuzi wa pamoja ili tushirikiane katika kuzitatua” alisema Nabalang’anya.

Nae mkuu wa msafara huo ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Jinsia katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Grace Mwangwa aliwaomba kuendelea na moyo huo thabiti wa kuwalea watoto hao.

“Wizara inawashukuru sana na inawaunga mkono, ustawi wa watoto ni kipaombele cha Wizara” alisema Mwangwa.

“Maadhimisho ya siku ya Wanawake huambatana na shughuli mbalimbali, hivyo siku ya leo ni mahususi kwa ajili ya kutembelea maeneo ya watu wenye mahitaji maalum…watatembelewa wafungwa katika Magereza, vituo vya kulelea Wazee, watu wenye ulemavu na watoto yatima” aliongeza.

Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamaii, Jinsia, Wazee na Watoto- Idara ya Ustawi wa Jamii, Verediana Kimaro alisema kuwa wizara kwa kushirikiana na wadau imeanza utaratibu wa kutoa bima za afya kwa vituo vya kulelea watoto.

“Tunataka watoto wote wawe na bima ya afya” alisema Kimaro.

Awali akitoa taarifaf upi ya kituo hicho, msimamizi wa kituo Sr. Aurea Kyara alisema kuwa kituo hicho kina watoto 63 wenye umri kuazia miaka mitatu hadi saba. Alisema kuwa watoto hao wanakabiliwa na changamoto ya bima kwa ajili ya matibabu, vyeti vya kuzaliwa na shule wanazosoma kuwa mbali na kituo hicho.

Aidha,  aliyataja mafanikio ya kituo kuwa ni baadhi ya watoto waliolelewa kituoni hapo kufikia hatua ya Vyuo na Vyuo Vikuu.

Mengine ni Mkoa kufanikisha baadhi ya watoto kupata vyeti vya kuzaliwa na jamii inayozunguka kituo kutoa ushirikiano mzuri.

Timu ya kima mama kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamaii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Sheria na Katiba, Halmashauri ya Jiji la Dodoma na wadau kutoka taasisi mbalimbali walipeleka zawadi kituoni hapo zikiwemo taulo za kike, sukari, sabuni, mafuta ya kula na kupaka, mikate, nguo, dawa za meno, dawa za kuulia mbu, pipi pamoja na vitu vingine.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.