• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yapongezwa kwa kujali elimu jumuishi katika shule za awali na msingi

Imewekwa tarehe: August 21st, 2023



SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepongezwa kwa kujali elimu jumuishi katika shule za awali na msingi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kutoa fursa kwa watoto wengi kusoma.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Awali na Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla alipoongoza zoezi la kutoa kadi za bima za afya na vifaa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Mlezi iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mwl. Myalla alisema “siku ya leo ni siku jumuishi ya kuhimiza elimu jumuishi kwenye shule zetu. Tunamshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kulisimamia hilo kwenye shule zetu kama ambavyo leo tumekusanyika hapa kugawa vifaa kwa wanafunzi wetu wenye mahitaji maalum kwa shule nane zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Tunaona kabisa ana nia ya dhati kuhakikisha na watoto wetu wenye mahitaji maalum wanapata elimu iliyo sawa na watoto ambao hawana mahitaji maalum”.

Alisema kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeandaa kadi za bima za afya 49 kati ya 100 kwa ajili ya kupata huduma za kiafya kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum. “Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imeandaa vifaa vya kufundishia na kujifunzia ili nao wapate elimu iliyo bora kwa watoto wetu wenye mahitaji maalum kupitia shule zetu zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Tunawashukuru wadau kwa kutoa vitimwendo kwa wanafunzi wetu wenye ulemavu. Tunatarajia wadau wa namna hii kuendelea kuiunga mkono halmashauri yetu. Huu ndiyo ushirikiano wa taasisi binafisi na serikali katika kuunga mkono maendeleo ya nchi yetu kupitia elimu” aliongeza Mwl. Myalla.

Akisoma taarifa fupi ya elimu maalum, Mkuu wa seksheni ya Elimu Maalum, Mwl. Issa Kambi alisema “tunaishukuru serikali ya awamu ya sita, kupitia Ofisi ya Rais, Tamisemi kwa kutenga kwenye bajeti ya mwaka 2023/2024 jumla ya shilingi 323,366,172 kwa ajili ya chakula cha wanafunzi wenye mahitaji maalum. Kila mwezi tunapokea jumla ya shilingi 26,947,181 kupitia ruzuku zinazoingizwa katika shule zenye wanafunzi wenye mahitaji maalum”.

Alisema kuwa katika bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia fedha za uendeshaji imetenga jumla ya shilingi 26,460,000 kwa ajili ya shughuli mbalimbali na ununuzi wa vifaa visaidizi na vifaa vya kufundishia na kujifunzia wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Akiongea kwa niaba ya maafisa elimu kata wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Afisa Elimu Kata ya Hazina, Mwl. Zaituni Mkoyi alisema “kwa niaba ya maafisa elimu kata wa shule hizi nane ambazo tumekutana hapa, naishukuru serikali na wizara zake kuona umuhimu na kuwajali watoto hawa ambao ni kundi maalum.  Nipongeze wazazi kuendelea kuwaleta watoto ili waweze kupata elimu ambayo ni haki yao. Niombe muwe chachu na ushawishi kwa wazazi wengine ambao bado wanaendelea kuwaficha watoto kama hawa”.

Mzazi wa mwanafunzi mwenye mahitaji maalum, Hincha Kweji alisema kuwa walimu wanaofundisha watoto wenye mahitaji maalum wanaupendo mkubwa. “Walimu hawa wamekuwa ni elimu kubwa sana kiasi kwamba wazazi tumefika mahali tukawapenda watoto wetu, ina maana walimu wametufundisha kuwapenda watoto wetu wenye mahitaji maalum” alisema Kweji.

Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoam ina jumla ya shule 61 zinazopokea watoto wenye mahitaji maalum, kati ya shule hizo 10 ni vitengo vya watoto wenye mahitaji maalum na moja ni maalum na shule 50 ni jumuishi. Jiji likiwa na wanafunzi 1,056 wenye mahitaji maalum.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.