• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yaridhishwa na kasi ya ujenzi wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI

Imewekwa tarehe: September 5th, 2022

Na. Asila Twaha, Dodoma

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameridhishwa na ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais - TAMISEMI na kuwaasa watendaji wa wizara hiyo kuendelea kusimamia kasi ya ujenzi wake ambalo tayari limefikia asilimia 54.

Majaliwa ametoa wito huo mapema leo Jijini Dodoma baada ya kupokea taarifa ya ujenzi na kukagua jengo hilo ambalo Serikali imetoa fedha kwa ajili ya muendelezo wa ujenzi wa Ofisi za Wizara zote za Serikali.

Amewapongeza mafundi na mkandarasi na kuwataka viongozi na watendaji wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuendelea kushirikiana na mkandarasi na mafundi ili kufikia lengo la Serikali la kujenga Ofisi zote za wizara hiyo katika Mji wa Serikali Mtumba.

“ Niwapongeze mafundi, taarifa inaonesha asilimia ya ukamilishaji ipo juu kuliko ilivyo kadiriwa”

Majaliwa amesema, azma ya Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ni kuendelea na kuuendeleza Mji wa Serikali pamoja na Makao Makuu ya Nchi, Jijini Dodoma kwa kujenga miundombinu ya barabara, miundombinu ya mifumo ya maji na kuendelea na ujenzi wa Wizara za Serikali ambapo zaidi ya bilioni 500 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa Wizara za Serikali lakini pia uwekezaji uliowekwa kwa kuendelezwa Dodoma.

Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya ujenzi Mkurugenzi wa Maendeleo ya Miundombinu Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mhandisi Gilbert Moga amesema, kwa mujibu wa kazi zilizotakiwa kukamilika hadi kufikia Agosti 30, 2022 ni umwagaji wa zege kwenye nguzo, ngazi na kuta kutoka kitako cha chini hadi sakafu ya pili ambayo ni asilimia 19.

Mhandisi Moga amesema hadi Septemba 5, 2022 hatua iliyofikiwa ni asilimia 54 ya mpango kazi ambapo Mkandarasi yupo mbele kwa asilimia 35.

Majaliwa amesema, ziara hiyo ni muendelezo wa kukagua ujenzi wa Makao Makuu ya Nchi ambapo alianza kwa kukagua ujenzi wa barabara ya mzunguko na kwamba ataendelea kukagua na kuona ujenzi wa majengo ya wizara mbalimbali yanayoendelea kujengwa ili kujiridhisha na maendeleo yake.

 Ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais, TAMISEMI unaoendelea kujengwa Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma unasimamiwa na Mtaalam Mshauri kutoka kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)


Chanzo: Tamisemi

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.