• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yashinda kesi ya hati ya makubaliano ya Muungano

Imewekwa tarehe: September 30th, 2020

Mahakama ya Jumuiya Afrika Mashariki imetupilia mbali madai ya kupinga uhalali wa Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao umeundwa Aprili 26, 1964 na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar (wakati huo) na Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika (wakati huo), ambapo shauri hilo lilifunguliwa na baadhi ya wanaharakati wa Zanzibar.

Wakili Mkuu wa Serikali Gabriel Malata ameeleza kuwa mahakama hiyo imetoa uamuzi huo baada ya kukubaliana na hoja zote za upande wa Serikali ikiwa ni pamoja na madai kuletwa nje ya muda, pamoja na uhalali wa mahakama kuhoji uhalali wa muungano huo.

Amesema Mahakama ya Afrika Mashariki imezaliwa kupitia makubaliano (The East African Community Treaty) ya mwaka 1999 na kuanza kufanya kazi mwaka 2000, hivyo mahakama hiyo haina mamlaka ya kuhoji Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964.

OFISI YA WAKILI MKUU WA SERIKALI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU USIKILIZWAJI NA UAMUZI WA SHAURI NAMBA 09/2016 KATIKA MAHAKAMA YA HAKI YA AFRIKA MASHARIKI BAINA YA RASHID SALUM ADIY NA WENZAKE 39,999 DHIDI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR, KATIBU MKUU KIONGOZI WA BARAZA LA MAPINDUZI LA ZANZIBAR NA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA WAKILI MKUU WA SERIKALI, TAREHE 29/9/2020 SAA 3:30 ASUBUHI

1.    UTANGULIZI

  • Mnamo tarehe 02 Novemba 2016, Bw. Rashid Salum Adily na wenzake 39,999 walikwenda kwenye Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki na kufungua Shauri Namba 09 ya Mwaka 2016 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi la Zanzibar wakihoji na kupinga uhalali wa vifungu na Hati ya makubaliano ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa sababu zifuatazo:-
  • Hati ya Makubaliano inayodaiwa kusainiwa tarehe 26/4/1964 baina ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar haipo (non existent)
  • Hati ya Makubaliano inayodaiwa kusainiwa tarehe 26/4/1964 baina ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar ni batili
  • Hati ya Makubaliano inayodaiwa kusainiwa tarehe 26/4/1964 baina ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar haijawahi kuridhiwa wakati wowote ule na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar.
  • Uwepo wa Jamhuri ya Muungano ni batili kwa sababu umetokana na Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ambao haujawahi ridhiwa na pande zote mbili za Muungano
  • Zanzibar ni Taifa huru na linalojitegemea kwani halijawahi ungana na Taifa lolote.
  • Hivyo, waliiomba Mahakama itoe tamko la kubatilisha Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao umetokana na Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar.
  • Kwa upande wa Serikali ambao ni wajibu maombi, waliwasilisha majibu ya Utetezi juu ya Uhalali wa kisheria wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar pamoja mapingamizi ya awali ya kisheria. Mapingamizi hayo ni;
  • Kwamba, Mahakama ya Afrika Mashariki haina mamlaka kisheria  kusikiliza hoja za kupinga uwepo wa Taifa la Tanzania lililotokana na Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar,
  • Kwamba, madai yamewasilishwa nje ya muda uliowekwa na Ibara ya 30(2) ya Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ya mwaka 1999.


2.    USIKILIZWAJI WA SHAURI

•    Shauri lilisikilizwa tarehe tarehe 6/7/2020 kwa njia ya Video ( Video Conference) ambapo wadai waliwakilishwa na Mawakili wa Serikali kutoka  Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wa Tanzania pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapunduzi ya Zanzibar ambao ni;

  1. Gabriel P. Malata- Wakili Mkuu wa Serikali
  2. Vicent Tango-Wakili wa Serikali Mkuu
  3. Ali. A. Hassan-Wakili wa Serikali Mkuu
  4. Juma Msafiri-Wakili wa Serikali Mkuu
  5. Mbarouk Othman Suleiman-Wakili wa Serikali Mwandamizi
  6. Stanley Kalokola-Wakili wa Serikali

•    Upande wa Walalamikaji uliwakilishwa na Wakili Rashid Mutola

HOJA ZA SERIKALI KATIKA MAPINGAMIZI YA AWALI:

•    Serikali ilipinga uwezo wa Mahakama kusikiliza Shauri linalohusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa hoja zifuatazo

  1. kwa mujibu wa Ibara ya 27 na 30 ya Mkataba wa Uanzishaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mhakama haina mamlaka kisheria kuhoji uhalali na uundwaji wa nchi yoyote ile kwani kufanya hivyo ni sawa na hata mahakama yenyewe kujihoji kuhusu uhalali wake kwani umetokana na uwepo wa nchi hizo zinazounda jumuiya ya Afrika Mashariki zikiwemo na Hoja ya msingi katika ibara tajwa ni kwamba Mahakama haina mamlaka ya kuhoji Muungano huo na kwa kwamba hoja za walalamikaji hazina mashiko mbele ya Mahakama hiyo.
  2. Mahakama haina mamlaka ya kusikiliza na kutafsiri vitendo, maamuzi yaliyofanywa na Taifa huru kabla ya kuanzishwa kwa jumuiya ya Afrika Mashariki na Taasisi zake ikiwemo Mahakama yenyewe
  3. Madai yameletwa nje ya muda wa siku sitini(60) kama inavyoelekezwa na ibara ya 30(2) ya Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

HOJA ZA WALALAMIKAJI KUHUSU MAPINGAMIZI YA AWALI.

Walalamikaji kupitia Bw. Rashid Mutola walipinga hoja za Serikali kwa hoja kwamba Mahakama ina mamlaka na malalamiko ya wateja wake yanahusu haki za binadamu kwani wakati wa kuanzishwa Muungano wananchi wa Zanzibar hawakushirikishwa. Aidha, walalamikaji walidai kwamba madai yao ni ya msingi.

Na hivyo waliomba mapingamizi ya Serikali yatupiliwe mbali na shauri liendelee kusikilizwa kwa wahusika kuendelea kutoa ushahidi kama ilivyokubaliwa kwenye Kongamano la pamoja (scheduling conference).

UAMUZI WA MAHAKAMA:

Shauri hili limetolewa uamuzi tarehe 29/9/2020 kwa njia ya Video (Video Conference). Katika Maamuzi yake, Mahakama imekubaliana na hoja zote za Serikali kuhusu kutokuwa na uhalali wa kisheria wa Mahakama kusikiliza Shauri hilo. Pamoja na mambo mengine, Mahakama imekubaliana na hoja zote za Serikali. Katika uamuzi wake Mahakama ilieleza mambo yafuatayo:-

Mahakama haina mamlaka ya kisheria kuhoji uwepo Taifa huru wa Jamhuri ya Muungano Tanzania ikiwa ni pamoja kutoka tafsiri ya maamuzi ya nchi mbili huru zilizounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambazo kwa mujibu wa Mkataba wa Uanzishaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Tanganyika na Zanzibar sio nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki

Mahakama imekubaliana na hoja kwamba, wadai hawana hoja yoyote dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ndiyo mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwani wadai wameshindwa kuthibitisha madai yao kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo wakati Hati za Muungano zinasajiliwa katika Umoja wa Mataifa na kutambuliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hakuna mapingamizi yaliyowasilishwa kupinga hati za Muungano kutoka kwa Tanganyika au Zanzibar.

Mahakama pia ilikubaliana na hoja madai yaliwasilishwa nje ya siku 60 zinazotajwa katika ibara ya 30(2) ya Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kuhusu gharama, Mahakama imeamua kila upande ubebe gharama zake kwa kuzingatia kwamba shauri hilo liliwasilishwa kwa kuzingatia maslahi ya Umma (public interest).

Mwisho, Shauri hili limetupiliwa mbali kwa hoja zilizotajwa hapo juu.

Imeandaliwa na

Gabriel Pascal Malata,

Wakili Mkuu wa Serikali,

Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali,

Dar es Salaam, 30 Septemba 2020.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.