• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yatangaza neema kwa wakulima wa zabibu Dodoma

Imewekwa tarehe: June 11th, 2022

Serikali kwa kupitia Wizara ya Kilimo imepanga kujenga vituo vitatu (Storage Facilities) vya kukusanya, kuchakata na kuhifadhi mvinyo ghafi wa zabibu mkoani Dodoma kwa lengo la kuokoa zabibu za wakulima zinazooza shambani kwa kukosa masoko kwa wakati.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Anthony Mavunde katika kikao cha wadau wa zabibu kilichofanyika katika ukumbi wa PSSSF Jijini Dodoma ambacho lengo lake kubwa ni kujadili muongozo wa usimamizi wa zao la zabibu kufuatia hatua inayoendelea ya uazishwaji wa Chama kikuu cha Ushirika wa wakulima wa zabibu.

“Changamoto kubwa inayowakabili wakulima wa zabibu ni kukosekana kwa soko la uhakika jambo ambalo hupelekea mkulima kuuza zabibu zake kwa bei ya hasara.

Uanzishwaji wa vituo hivyo cha uchakataji na uhifadhi wa mchuzi wa zabibu utampa uhakika mkulima kutopoteza mazao yake ya shambani kwa kuoza na hivyo kupelekea kuuza zabibu kwa bei ya chini kwakuwa sasa ataweza kuuza mvinyo ghafi utakaohifadhiwa kusubiri soko.

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuwainua wakulima wakiwemo wa zabibu kwa kukipa Kilimo kipaumbele cha juu, dhamira hii inaonekana kwa namna ambavyo bajeti ya kilimo imekwenda juu kutoka shilingi Bilioni 294 mpaka kufikia shilingi Bilioni 751.

Katika kuhakikisha wakulima wa zabibu wanazalisha kwa tija na weledi  Serikali itasimamia mafunzo ya wataalam na wakulima juu ya zao la zabibu na ikiwezekana kwenda kujifunza katika nchi zinazofanya vizuri kwenye kilimo cha zabibu ili wakulima watakaopata fursa ya kujifunza wakasaidie kufundisha wakulima wengine” Alisema Mhe. Mavunde.

Wakati huo huo Mhe. Mavunde amewataka wadau wa zabibu kujadili kwa uwazi muongozo wa uzalishaji, masoko na uchakataji wa zabibu ili yapatikane mawazo yenye nia ya kujenga na hatimaye kuleta maendeleo kwenye zao hilo.

Awali akitoa salamu za mkoa wa Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Mwanahamisi Mukunda amesema ana imani kubwa na uwezo wa Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe  pamoja Naibu Waziri Mhe. Anthony Mavunde katika kuwasaidia wakulima wa zabibu mkoani Dodoma.

Aliongeza kuwa, kwa kasi ya viongozi hao pamoja na dhamira ya Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan changamoto za wakulima wa zabibu zitatatuliwa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.