• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yatoa ahadi kwa wajane nchini

Imewekwa tarehe: June 24th, 2019

Serikali itaendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya mirathi na uandishi wa wosia ili kuondoa migogoro inayowakabili wajane nchini kutokana na kudhulumiwa haki zao.

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akiwahutubia mamia ya wananchi katika maadhimisho ya siku ya wajane duniani iliyofanyika kitaifa katika uwanja wa Nyerere square jijini Dodoma jana.

Dkt. Ndugulile alisema “sisi kama serikali kupitia Idara kuu ya Maendeleo ya jamii na wadau wote tuendelee kutoa elimu kwa jamii hususani masuala yanayohusu mirathi na kuacha wosia. Watu wengi hawajui haki zao, wanakutana huko wanaishi pamoja hakuna cheti”. Watu wote wenye ndoa za asili wasajiri ndoa hizo na kupatiwa hati za usajili, alishauri.

Aidha, wadau na taasisi nyingine ambazo zinatoa ushauri wa kisheria wametakiwa kwenda kutoa elimu kwa jamii juu ya masuala ya mirathi. “Twende tukatoe elimu kwenye jamii kuhusiana na taratibu za mirathi, nini unachotakiwa kufanya wewe mjane, badala ya kukimbilia kulia kwa uchungu, huku nyuma watu wanakuzunguka, wanaanza kutafuta hati za nyumba, wanaenda kuchukua cheti cha kifo wanaenda kukimbilia nyaraka zote nyeti ambazo mwisho wa siku zitakuja kukupa shida katika kusimamia mirathi yako” alisema Dkt. Ndugulile.

Akiongelea maadhimisho hayo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Idara kuu ya Maendeleo ya jamii, Dkt. John Jingo alisema kuwa maadhimisho hayo yamewakutanisha wajane kutoka karibu mikoa yote Tanzania na Wizara yake imewajengea uwezo kuhusu masuala ya ujasiriamali na stadi za maisha.

Maadhimisho ya siku ya wajane duniani yamefanyika kitaifa kwa mara ya kwanza nchini katika jiji la Dodoma wakati dunia ikikadiliwa kuwa na zaidi ya wajane milioni 258. Kati ya wajane 10, mjane mmoja anaishi katika umasikini wa kutupwa.

Mkazi wa Mkoa wa Mwanza, Veronica Nyabumera aliiomba serikali kusaidia uanzishaji wa Sera ya taifa ya wajane itakayowatambua wajane kama kundi maalum katika jamii. Kuanzishwa kwa sera ya Taifa kwa ajili ya wajane kutasaidia kutoa msukumo kwa jamii juu ya haki na madhira wanayopitia wajane, aliongeza. Alisema kuwa kundi hilo limekuwa likidhurumiwa mali pindi wenzi wao wanapofariki. Aidha, Nyabumera alishauri kuwa vifo vya wanaume vitambuliwe kuwa vinatokana na mapenzi ya Mungu kama vilivyo vifo vya wanawake. “Pendekezo langu vifo vya wanaume navyo vitambuliwe kuwa vinatokana na mapenzi ya Mungu kama vilivyo vifo vya wanawake na siyo kurogwa. Jambo hilo ndilo linalosababisha wajane tunakosa haki zetu baada ya kufiwa na waume zetu” alisema Nyabumera kwa uchungu.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile (katikati mwenye kaunda suti) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali, dini na baadhi ya wawakilishi wa wanawake wajane nchini

Naibu Waziri Ndugulile akifurahia baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na wanawake wajane.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.