• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yaunda timu kutafiti zao la zabibu

Imewekwa tarehe: February 14th, 2020

Serikali imeunda timu ya watu 12, ambayo itafanya utafiti wa zao la zabibu kama linaleta hasara au faida kwa mkulima na serikali.

Timu hiyo itafanya kazi ndani ya siku 10 pia imeagizwa kujua magonjwa yanayoathiri zao hilo. Kauli hiyo ilitolewa Februari 11, 2020 na Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, alipokuwa akizungumza na wadau wa zao hilo jijini hapa.

Alisema zao hilo ambalo linalimwa mkoani Dodoma linakua kwa kudra za Mwenyezi Mungu, ndio maana ameamua kuunda timu hiyo ambayo itawasilisha ripoti wizarani.

Bashe alisema kuwa zao hilo ndio uti wa mgongo wa wakazi wa Dodoma hivyo kuna haja ya kuweka mpango mkakati kwa ajili ya kuinua zao hilo.

"Kamati ya watu 12 itakayoongozwa na Mwenyekiti Gungu Mibavu, kutoka Ofisi ya DPP, Sera na Mipango ambapo wote watafanya utafiti kwa muda wa wiki moja na kuwasilisha ripoti itakayoletwa na kamati hii itatusaidia kujua wakulima wa zabibu wako wangapi? Changamoto za wakulima, wazalishaji na wasindikaji, hivyo itatusaidia katika mikakati yetu," alisema Bashe.

Alisema mkakati mwingine wa serikali ni kufufua mabwawa yote yaliyotengenezwa kwa ajili ya umwagiliaji wa zabibu katika wilaya tatu zinazolima zao hilo ambazo ni Bahi, Chamwino na Dodoma.

Bashe aliwataka wadau wa kilimo hicho kuunda vyama vya ushirika ili kupata fursa kwenye taasisi za fedha.

Naye Mkurugenzi wa Doniya Estate, ambaye ni msindikaji wa zao la zabibu, Catherine Mwambe, alisema kuwa suala la kodi limekuwa kikwazo kikubwa kwa wazalishaji wa mvinyo.

"Kwa siku moja zinakuja taasisi zaidi ya tano kila moja inakuja kuchukua kodi, hata faida hatupati, maana hela yote inaishia kwenye hizo kodi," alisema Mwambe.

Alisema, gharama za uzalishaji ziko juu na soko la zabibu nchini bado na kuiomba serikali kuingilia kati na kuweka mazingira rafiki ya biashara ya zao hilo.


Chanzo: www.kilimo.go.tz


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.