• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yawashukuru wadau wa maendeleo sekta ya Afya

Imewekwa tarehe: November 20th, 2019

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewashukuru wadau wa maendeleo katika sekta ya afya wanaochangia Mfuko wa Afya wa pamoja kwa kuchangia pesa kiasi cha shilingi bilioni 127 kwa ajili ya kutoa na kuboresha huduma za afya.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu alipofanya ziara ya pamoja na wadau hao katika Kituo cha Afya cha Hombolo Jijini Dodoma kukagua ujenzi wa majengo matano ambayo ni nyumba ya mganga, Maabala, Chumba cha kuhifadhia maiti, Wodi ya kinamama pamoja na Chumba cha Upasuaji.

“Wadau hawa wametupatia shilingi Bilioni 127 kwaajili ya kuboresha huduma za afya, kati ya hizo, bilioni 104 tunazileta kwenye Halmashauri za wilaya pamoja na Sekretarieti za Mikoa ili kuendesha huduma za afya, kwa hiyo hela nyingi zinakuja huku chini kwenye zahanati, kwenye vituo vya afya, kwenye hospitali za wilaya na kule juu tutaweka hela ndogo”

Waziri Ummy amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya Afya Duniani wataendelea kuhakikisha sekta hiyo inapata mafanikio kwa kuboresha huduma za Afya Nchi nzima.

Nae Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi ameishukuru Wizara ya Afya pamoja na wadau kwa fedha hizo kwani kwa kiasi kikubwa zimekua zikisaidia kuboresha huduma za Afya hasa katika ngazi ya Zahanati na Vituo vya Afya.

“Jiji la Dodoma tumepokea shilingi milioni 500, na tukazitumia vizuri sana, kwa sababu tulipaswa kujenga majengo matano ambayo yote yamekamilika, lakini sisi hatukuwa nyuma tukasema licha ya kupokea fedha hizi tukaongeza wenyewe milioni 193 kupitia mapato ya ndani, ambapo katika fedha hizo tumetumia milioni 63 kwa ajili ya kujenga Wodi ya watoto, kwa hiyo leo hii zahanati ya Hombolo ina Wodi ya kinamama na Watoto.” alisema Kunambi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu (kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi alipotembelea Kituo cha Afya cha Hombolo kukagua ujenzi wa miundombinu ya majengo ya kituo hicho.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.