• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yawatoa hofu Watanzania kuhusu ugonjwa wa Corona

Imewekwa tarehe: January 28th, 2020

Serikali imewataka Watanzania kuwa watulivu kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa homa ya corona uliotokea China, na kueleza kuwa hadi sasa hakukna Mtanzania aliyeathiriwa na maradhi hayo.

Hadi sasa ugonjwa huo ambao ulianzika katika Jiji la Wuhan nchini China umeshaua watu zaidi ya watu 80 na zaidi ya 2,000 wakiwa wameambukizwa.

Tangu kugundulika kwa ugonjwa huo, mamlaka ya China imesitisha safari za ndege kwa raia wake wanaotoa na kuingia nchini humo.

Akitoa ufafanuzi kuhusu Watanzania waishio nchini China, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi, aliwataka wawe watulivu, makini na kupenda kuwa na subira ya kupata maelezo au maelekezo na ufafanuzi rasmi wa serikali.

“Watanzania tunaomba muwe na subira ya kupata maelezo au maelekezo na ufafanuzi rasmi wa serikali pale kunakotokea jambo badala ya kukimbilia kwenye mitandao na uvumi ili kuondoa kueneza hali ya taharuki kwa wananchi bila ya kuwa na uhakika,” alisema Prof. Kabudi.

Alisema Tanzania ina wanafunzi takribani 4,000  na kwamba katika mji wa Wuhan wapo 400.

Alisema kwa mujibu wa taarifa ya Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki, ameihakikishia serikali kuwa mpaka sasa hakuna Mtanzania yoyote aliyeathiriwa ama kukumbwa na maradhi hayo.

Alisema Tanzania inaendelea kufuatilia kwa ukaribu kujua maendeleo na hali za Watanzania wanaoishi jimboni Wuhan na China kwa ujumla.

Prof. Kabudi aliwataka Watanzania kuwa makini na suala la kutoa taarifa zisizo rasmi au za uvumi kwa sababu kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

WATALII 500 WAKWAMA KUJA

Wakati huohuo, mlipuko wa ugonjwa huo umesababisha kusitishwa kwa safari ya watalii zaidi ya 500 waliotarajiwa kuja nchini katika kipindi cha Februari na Machi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Jaji mstaafu, Thomas Mihayo, alisema watalii hao walitarajiwa kuingia nchini Februari 24 na Machi 2 mwaka huu na ndege za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).

“Napenda kuchukua fursa hii kwa masikitiko makubwa kuwajulisha safari za ndege maalumu za ATCL za kuleta wageni, zilizokuwa zimepangwa kufanyika Februari na Machi, zimeahirishwa baada ya serikali ya China kuzuia wananchi wake kusafiri nje ya nchi hiyo, kutokana na mlipuko wa ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona,” alisema Jaji Mihayo.

Kwa mujibu wa taarifa ya TTB iliyotolewa Desemba mwaka jana, Tanzania ilikuwa inatarajia kupokea watalii zaidi ya 500 kwa awamu mbili kutoka China katika kipindi cha Februari 24 na Machi 2 mwaka huu.

Ndege ya ATCL aina ya Boeing 787-8 Dreamliner ndiyo ilitarajia kwenda kuwachukua watalii hao na kuwaleta nchini kwa ajili ya kufanya utalii katika vipindi hivyo viwili.

Chanzo: www.ippmedia.com


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.