• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Shirikianeni kutoa taarifa sahihi za utekelezaji wa maamuzi mbalimbali yanayokubaliwa katika vikao - RC Senyamule

Imewekwa tarehe: July 7th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Dodoma amewataka Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Makatibu Tawala Wasaidizi wa Idara mbalimbali za Ofisi ya Mkoa wa Dodoma kushirikiana na kutoa taarifa sahihi za utekelezaji wa maamuzi mbalimbali yanayokubaliwa katika vikao mbalimbali vya Utekelezaji ili kufanikisha utekeleza kikamilifu wa Miradi ya Boost ili kurahisisha utendaji kazi na kukamilisha Miradi hiyo kwa wakati.

Senyamule ameyasema hayo katika kikao kazi cha kujadili Utekelezaji wa Bajeti ya 2022/2023  na Utekelezaji wa Mpango kazi wa Mwaka wa Fedha 2023/2024 kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jengo la Mkapa kufuatia kutokamilika kwa miradi kwa wakati kama ilivyoelekezwa.

Aidha, Senyamule amewataka Viongozi hao wa ngazi ya Wilaya kuendelea kutunza Mazingira kwa kuanza maandalizi ya kupanda miti na kutenga maeneo ya kuoteshea vitalu vya Miche ya miti kwaajili ya  kupanda wakati wa Msimu wa Mvua unapokaribia ili kuwe na miche ya kutosha kwa kila Halmashauri kupanda miti milioni moja na laki tano kwa Mwaka kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali.

"Katika kuendelea kukijanisha Mkoa wetu na kutunza Mazingira yetu tuanze mapema maandalizi ya kuandaa vitalu vya miche na kila wilaya iwe na Miche ya kutosha isiyopungua milioni moja na laki tano kama agizo lilivyotolewa na Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hapa nisisitize kuwa katika kila wilaya nitakayofanya ziara kuanzia mwezi huu nitakagua vitalu hivyo vilevile hakikisheni mnatenga maeneo kwa ajili ya kunufaika na biashara ya hewa Ukaa na kila Wilaya angalau iwe na maeneo matatu kama tulivyokubaliana hapo awali". Amesisitiza  Senyamule

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Dodoma Bw. Gift Kyando ametoa rai wilaya zilizokamilisha ujenzi wa Shule na madarasa kupitia fedha za mradi Boost kuanza usajili wa Shule hizo mapema ili zianze kupokea wanafunzi ifikapo Mwezi Januari 2024.

"Kwa Halmashauri ambazo zimekamilisha ujenzi wa Miradi hii zinatakiwa kuanza usajili ili mwakani tuanze kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza na kuwahamishia wanafunzi wa kidato cha pili na tatu kwa wale wanaotoka maeneo ya mbali na Shule wanaposoma kwa sasa hii itawarahisishia masomo yao".

Katika kuendelea kuboresha na kuweka miundombinu rafiki kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu Bw. Kyando amewaomba wasanifu ramani za Majengo ya Miradi hiyo kuandaa ramani rafiki kwa wanafunzi Wenye Ulemavu wa viungo na zitakazotumia gharama ndogo huku zikiwa na Ubora unaohitajika.

Kikao hiki cha kujadili utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2022/23 na Utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka 2023/24 pia kimejadili miradi ya elimu kupitia fedha za boost na SEQUIP. Pia, wajumbe walipata fursa ya kutambulishwa katika program endelevu ya usafi wa mazingira na upatikanaji wa maji Vijijini na Mfumo wa Dharura wa Rufaa wa usafirishaji wa wajawazito na watoto wachanga.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.