• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Shule ya mtaala wa kiingereza kutoa elimu bora Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: August 17th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA


HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inajenga shule ya msingi ya mtaala wa kiingereza ili kutoa elimu bora itakayowasaidia wanafunzi kupata maarifa na umahiri katika masomo ili wawe wataalam wa nyanja mtambuka nchini na kulisaidia taifa kufikia mapinduzi ya kiuchumi.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Myalla alipokuwa akisoma taarifa ya ujenzi wa shule ya msingi ya mtaala wa kiingereza kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Sahili Geraruma katika eneo inapojengwa shule hiyo Kata ya Dodoma Makulu jijini hapa.

Myalla alisema kuwa lengo la mradi huo ni kutoa elimu bora itakayowasaidia wanafunzi kupata maarifa na ujuzi utakaowawezesha kuwa wanafunzi mahiri katika masomo. “Elimu hiyo itawawezesha kuwa wataalam katika nyanja mbalimbali ndani na nje ya nchi na kusaidia taifa kufikia mapinduzi ya kiuchumi yatakayoiwezesha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati. Lengo lingine ni kuwezesha wanafunzi na walimu kuwa na mahali pazuri pakujifunzia na kufundishia. Pamoja na kuongeza uandikishaji wa wanafunzi wa awali kutoka 13,056 kwa mwaka 2022 hadi 17,556 kwa mwaka 2025. Pia kuongeza uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza kutoka 19,494 kwa mwaka 2022 hadi 23,994 kwa mwaka 2025” alisema Myalla.

Akiongelea hali ya utekelezaji wa mradi huo, alisema kuwa mradi ulianza tarehe 20.05.2022 kwa halmashauri kupata eneo lililopimwa katika kiwanja namba 20 na 21 Kitalu C Mapinduzi East chenye ukubwa wa Hekta 3.71 sawa na Ekari 9.17 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule na viwanja vya michezo. “Hali ya utekelezaji kwa upande wa vyumba vinane vya madarasa viko hatua ya renta, matundu 32 ya vyoo vya wavulana na wasichana hatua ya kupaua na jengo la utawala hatua ya skimming. Hadi sasa jumla ya shilingi 298,243,133.10 zimeshatumika ikiwa ni pamoja na ununuzi wa vifaa vya ujenzi, malipo ya mafundi, gharama za uingizaji umeme na maji eneo la mradi, gharama za upimaji wa nondo, tofali, kokoto na mchanga. Halmashauri inatarajia kukamilisha ujenzi wa mradi huu ifikapo mwezi Oktoba, 2022” alisema Myalla.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilipokea jumla ya shilingi 750,000,000 tarehe 30 Machi, 2022 kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa ajili ya ujenzi wa shule ya mtaala wa kiingereza.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.