• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Sekondari ya Bihawana yapongezwa kusimamia Milioni 240 ujenzi madarasa, mabweni

Imewekwa tarehe: October 18th, 2022

Na. Theresia Nkwanga, DODOMA

KAMATI ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepongeza usimamizi wa mradi wa ujenzi wa madarasa mawili na mabweni mawili katika shule ya sekondari ya Bihawana kwa gharama ya shilingi 240,000,000.

Pongezi hizo zilitolewa na kiongozi wa kundi namba moja, Diwani Gombo Dotto alipoongoza kundi hilo kutembelea na kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa madarasa mawili na mabweni mawili ya shule ya sekondari Bihawana iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Diwani Dotto alisema “mradi tumeukagua ni mzuri unaakisi fedha zilizotumika. Taarifa ya mradi tumeisoma imeandaliwa vizuri, niwapongeze kwa usimamizi mzuri wa mradi huu. Ni matumaini yangu mtaukamilisha haraka sababu vifaa vyote mnavyo pia nimpongeze Afisa Elimu Sekondari, Upendo Rweyemamu kwa utendaji wake mzuri wa kazi na usimamizi”.

Aidha, alishauri kutumia ‘Marine board’ badala ya mbao ili kupunguza gharama za ujenzi. ‘Marine board’ huweza kutumika zaidi ya mara moja tofauti na mbao ambazo zikimaliza kazi haziwezi kutumika tena kutokana na kupinda, aliongeza.

“......kama majengo ni mengi ni vema mfikirie kutumia “marine board” ambazo gharama yake ni nafuu ukilinganisha na mbao, pia mbao zinatumika nyingi sana kwenye ujenzi tofauti na ‘marine’ na zikishatumika ni ngumu kuzitunza kwaajili ya matumizi ya badae mwisho wa siku zinakosa pakwenda zinaishia kutupwa au kutumika kama kuni”.

Nae Mkuu wa shule ya sekondari Bihawana, Liberatus Ntilema alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutatua changamoto za msongamano wa wanafunzi katika madarasa na mabweni. Vilevile, aliushukuru uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa maelekezo makini na ushauri wa mara kwa mara katika ujenzi unaoendelea. “Mradi huu unagharimu kiasi cha shilingi milioni 240,000,000, fedha za Mpango wa Uboreshaji wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP)” alisema Ntilema.

Akiongelea changamoto zinazoukabili ujenzi huo, Ntilema alizitaja kuwa ni kuchelewa kwa kuwekewa vifungu vya malipo ya mradi wa SEQUIP hali iliyosababisha fedha za mradi kuvuka mwaka wa fedha 2021/22 bila kutumika. Nyingine ni ongezeko la bei kwa vifaa vya ujenzi na gharama kubwa za usafiri kutoka mahali vifaa vilipo hadi shuleni. Kukosekana kwa fedha ya ufatiliaji wa maswala yote ya ujenzi na uchelewaji wa kufunguka mfumo wa FFARS kwa mwaka mpya wa fedha 2022/2023 kumechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza kasi ya ujenzi, aliongeza. 

Alimalizia kwa kuelezea changamoto zinazoikabili shule ya sekondari Bihawana kuwa ni shule kutokuwa na walimu wa kutosha kulingana na idadi ya wanafunzi. Nyingine ni shule kutokuwa na jiko la kupikia na shule kutokuwa na bwalo kubwa linaloendana na idadi ya wanafunzi na shule kukosa ukumbi wa mikutano.

Shule ya sekondari Bihawana ina jumla ya wanafunzi 838 ambao wote ni wavulana wa kidato cha Tano na Sita katika tahasusi za CBA, CBG, HGL, PCB na PCM kati ya wanafunzi hao 361 (41%) ni wa kidato cha Tano na kidato cha Sita ni 477 (58.9%) ikiwa na jumla walimu 27 kati ya hao wa kiume ni 19 na wa kike ni 8.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.