• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Shule za vijijini zapata afueni, ajira 13,000 za Walimu

Imewekwa tarehe: November 27th, 2020

KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema Serikali imewapangia waalimu wengi zaidi wa shule ya msingi katika shule za vijijini ambako ndiko kwenye upungufu mkubwa wa waalimu.

Akiongea na vyombo vya habari leo kuhusu ajira mpya za waalimu wa shule za Msingi na Sekondari pamoja na mafundi sanifu wa maabara, Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa kwa upande wa shule za msingi  upangaji wa waalimu umefanyika kwa lengo  la kuboresha  uwiano wa waalimu kwa wanafunzi.

Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa asilimia 60 ya walimu wote walioajiriwa wamepelekwa katika shule za msingi hasa za vijijini ambako ndiko kwenye uhitaji mkubwa wa waalimu nchini.

Ameendelea kufafanua kuwa Serikali imeweka kipaumbele kuajiri waalimu kwa ajili ya shule za sekondari zenye mchepuo wa sayansi na Hisabati, ufundi, kilimo na maarifa, maarifa ya nyumbani, lugha ya kiingereza, kichina na kifaransa.

Amesema kuwa walimu wa masomo mengine wamepangwa kulingana na upungufu uliopo ambapo kipaumbele ni shule ambazo hazina walimu wa masomo husika.

Mhandisi Nyamhanga amesema pia wamezingatia shule zenye mahitaji maalum ambako waalimu 481 wameajiriwa kwa ajili ya shule hizo na kuwa suala la umri wa ajira za Serikali limezingatiwa na waalimu waliopata ajira ni wale waliomaliza chuo mwaka 2014 mpaka 2019.

Aidha, Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa waajiriwa wapya  wa uwaalimu  wa shule za Msingi na Sekondari wanatakiwa kuhakikisha wanaripoti katika vituo walivyopangiwa ndani ya muda wa siku 14, kinyume na hapo watakuwa wamepoteza  nafasi zao na zitajazwa na waombaji wengine.

“waajiriwa wapya  wanatakiwa  kuripoti kazini  kuanzia tarehe 1 hadi  tarehe 14 Desemba 2020  watakaoshindwa kuripoti nafasi zao zitajazwa na waombaji wengine wenye sifa waliopo kwenye kanzidata ya Ofisi ya Rais –TAMISEMI”, amesisitiza Mhandisi Nyamhanga.

Vile vile amewaagiza  wakurugenzi wa Halmashauri ambao walimu hao wamepangiwa kuwapokea na kuwawezesha  kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma.

Hata hivyo amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanatoa taarifa ya kuripoti waajiriwa hao na kuzijaza kwenye mfumo wa kielektroniki baada ya kila mtumishi kupokelewa katika kituo cha kazi.

“Kamilisheni taratibu za ajira haraka ili walimu hawa waingizwe katika mfumo wa malipo ya mshahara (payroll) mapema iwezekanavyo”, ameelekeza Mhandisi Nyamhanga.

Tarehe 7 Septemba, mwaka huu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alitoa kibali cha ajira mpya za walimu 13,000 wa shule za Msingi na Sekondari pamoja na Mafundi Sanifu wa Maabara za Shule.

Kuona Orodha bofya hapa: TAARIFA YA ORODHA YA MAJINA NA VITUO VYAO



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.