• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Siku ya Sheria Rais apongeza matumizi ya TEHAMA, aahidi fedha za ujenzi wa mahakama jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: February 6th, 2020

Aliyoyasema Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Naipongeza Sekta ya Sheria na Mahakama nchini kwa kupata mafanikio makubwa ikiwemo kupungua kwa muda wa usikilizwaji wa kesi, kuimarisha matumizi ya TEHAMA pamoja na kuanzisha Mahakama zinazotembea.

Matumizi ya TEHAMA yamepunguza utoaji na upokeaji wa rushwa pia yameongeza kasi ya ukusanyaji wa maduhuli kutoka shilingi Bil.1.6 kwa mwaka 2017 hadi shilingi Bil.2.6 mwaka 2019.

Mafanikio ya Mahakama pia yamechangiwa na uamuzi wa Serikali wa kuteua Majaji 11 wa Mahakama ya Rufani, Majaji 39 wa Mahakama Kuu pamoja na kuajiri Mahakimu wapya 396.

Uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi umeondoa dhana iliyokuwa imejengeka miongoni mwa wananchi kuwa mapambano ya rushwa nchini yamekuwa yakiwalenga wananchi wa chini na kuwaacha vigogo.

Tangu Mahakama hii ianzishwe mwaka 2016 jumla ya Mashauri ya uhujumu uchumi 119 yamesajiliwa na mashauri 89 yamemalizika ambapo faini ya sh.Bil 13.6 na fidia ya Bil. 30.6 zimetolewa.

Nakuhakikishia kuwa tutakupatia fedha za kujenga Mahakama ya Jijini Dodoma, pia kati ya watumishi 268 uliowaomba, tutaajiri watumishi 200 ili wakafanye kazi katika Mahakama mpya zinazojengwa.

Katika magereza yetu kuna jumla ya wafungwa 13,455 na mahabusu 17,632 hii inaonesha kuna ucheleweshwaji wa kesi hivyo wapelelezi hakikisheni mnaharakisha upelelezi kwani mnawanyima watu haki.

Bado kuna changamoto ya migogoro ya ardhi na dhuluma kwa wanawake hasa wajane, sina uhakika kama Mabaraza ya Ardhi yanafanya kazi vizuri pengine yapo chini ya Wizara ya Ardhi lakini lawama zinapotolewa zinarudi kwa Mahakama hivyo migogoro hiyo ifanyiwe kazi.

Serikali imepeleka Muswada wa Sheria ya Usuluhishi ili kufuta Sheria hizo za mwaka 1932, tunaamini sheria mpya itaziwezesha Mahakama zetu kufanya usuluhishi na tutaweza kuendana na mikataba mbalimbali ya kimataifa tuliyosaini.

Aliyoyasema Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Hamis Juma

Siku ya Sheria ni muda mzuri kwa wananchi kukumbushana umuhimu wa Katiba na Sheria katika kuwawezesha Watanzania kuendelea kuishi pamoja katika nchi huru na kutafakari namna ambayo Sheria itatumika kuwezesha kufanikisha ukuaji wa uchumi.

Kauli mbiu ya mwaka huu inawataka watumishi wa umma walio na majukumu ya kutekeleza sheria mbalimbali wajitathimini kama wanatumia sheria na taratibu za mahakama sio kwa lengo la kuweka vikwazo bali kuendeleza biashara na uwekezaji.

Tumesimika vifaa vya mawasiliano kwa njia ya video katika baadhi ya ofisi zetu ambapo hadi sasa mashauri 60 ya Mahakama ya Rufani  yamesikilizwa kwa kutumia mfumo huo pamoja na kusikiliza mashahidi waliopo nje ya Tanzania.


Chanzo: IDARA YA HABARI - MAELEZO



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.