• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Siri ya mafanikio jiji la Dodoma, Meya Prof. Mwamfupe afunguka

Imewekwa tarehe: June 9th, 2020

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitano tangu serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani kutokana na umoja wa Baraza la Madiwani na watendaji jambo lililoiwezesha kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe wakati akihutubia Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo kabla wa kulivunja rasmi tukio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha Mipango Dodoma.

Prof. Mwamfupe alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepiga hatua kubwa katika utoaji huduma bora kwa wananchi. Alisema kuwa jukumu kubwa la Halmashauri ni kutoa huduma bora kwa wananchi, kama tulivyosikia taarifa ya mafanikio ya Halmashauri iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Jiji. “Mafanikio yetu haya makubwa yanatokana na ukweli kuwa tumedumu wamoja kama Baraza la Madiwani. Mafanikio haya ni matokeo ya uongozi bora, amani na uwazi. Shukrani kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Magufuli kwa kutoa dira kwa taifa na kuhimiza watumishi na wananchi kufanya kazi. Lakini wakati huohuo, serikali hii imejipambanua kutokubembeleza watumishi wazembe. Kwa uzito huohuo, tunamshukuru kwa kutupa Makao Makuu Dodoma, tunamhakikishia kuwa tutaendelea kutekeleza wajibu wetu wakuwahudumia wananchi” alisema Prof. Mwamfupe.

Akiwasilisha taarifa ya mafanikio ya shughuli za Halmashauri kuanzia mwaka 2014/2015 hadi 2019/2020, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alisema kuwa Halmashauri imeendelea kupata mafanikio makubwa katika utoaji huduma bora kwa wananchi kupitia idara, vitengo na mamlaka zilizopo. Alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya serikali ya awamu ya tano Jiji la Dodoma limefanikiwa kuongeza ukusanyaji mapato kwa asilimia 1,349. “Jiji la Dodoma limeweza kuongeza na kukusanya mapato ya ndani kutoka bajeti ya shilingi 4,554,075,181 kwa mwaka 2015/2016 hadi shilingi 66,010,324,746 kwa mwaka 2019/2020 sawa na ongezeko la asilimia 1,349” alisema Kunambi.

Akiongelea hoja za ukaguzi, alisema kuwa Jiji la Dodoma limeweza kujibu na kupunguza hoja za ukaguzi zilizotolewa na CAG kutoka hoja 161 mwaka wa fedha 2015/2016 hadi hoja 46 mwaka 2018/2019 sawa na asilimia 71. Alisema kuwa kuanzia mwaka 2016/2017 hadi 2018/2019 Halmashauri ya Jiji imeendelea kupata hati safi ya ukaguzi.  

Mkurugenzi huyo alisema kuwa mafanikio ya miaka mitano ya serikali ya awamu ya tano yanatokana na juhudi za pamoja kati ya serikali kuu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wananchi pamoja na wadau waliohusika katika kuchangia michango mbalimbali ya maendeleo.

Katika salamu za Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini, Patrobas Katambi alilipongeza Baraza la Madiwani chini ya uongozi wa Mstahiki Meya kwa kazi nzuri. “Mkurugenzi wa Jiji amefanya kazi kubwa inayoonekana kwa ushirikiano na menejimenti yake na taasisi zote jijini hapa” alisema Katambi. Aidha, alieleza matarajio yake kuwa Halmashauri itaendelea kutatua changamoto zitakazojitokeza katika kuwatumikia wananchi.  

Kwa upande wake Ephrahim Matonya mwananchi aliyekuwa akifuatilia mkutano wa Baraza la Madiwani moja kwa moja kupitia njia ya mtandao alisema kuwa Jiji la Dodoma linaonesha mafanikio yajayo. Kwa miaka hii michache Dodoma kuna maendeleo makubwa aliongeza. “Zamani watu walikuwa wakiondoka kutoka Dodoma kwenda mikoa mingine, sikuhizi tunaona watu wengi wanakimbilia Dodoma” alisema Matonya.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limevunjwa rasmi na majukumu yake kukasimiwa kwa timu ya wataalam ya Halmashauri hiyo kwa kipindi chote hadi baraza lijalo litakapoapishwa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.