• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Spika Ndugai afunguka tozo ya miamala

Imewekwa tarehe: July 23rd, 2021

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, ameweka wazi kuhusu tozo ya miamala katika simu kwa kusema kuwa Bunge ndio liliamua na kupitisha na wale ambao wanapinga wanatakiwa kutoa mawazo mbadala ya nini kifanyike wakati akisisitiza lengo ni ifikapo mwaka 2025 Tanzania liwe Taifa tofauti katika suala la maendeleo.

Msimamo huo aliutoa katika kikao kazi cha viongozi wa Mkoa na wilaya zote za Dodoma kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na kufanyika katika ukumbi wa Kitivo cha Teknolojia ya Habari na Elimu Angavu katika Chuo kikuu cha Dodoma.

Akifafanua kuhusu adhima ya wabunge kuona baadhi ya mambo ya kimaendeleo yanasonga mbele alisema “Sisi pale Bungeni tumekaa na kufikiri sana kama watumishi wenu namna gani tunaweza kumaliza baadhi ya mambo ili tusonge mbele, tunataka ifikapo mwaka 2025 kisiwepo kijiji Tanzania nzima ambacho hakina huduma ya Umeme, ni lengo kubwa. Sasa tuna lengo la kuhakikisha kwamba kumtua ndoo mama kichwani ni jambo ‘reality’ (halisi) kupeleka maji vijiji vyote, tuna uhaba mkubwa sana wa madarasa ya shule za msingi na sekondari ni uhaba mkubwa kweli kweli, tunataka jambo hilo liwe historia. Tuna uhaba mkubwa sana wa madawati… hatutaki kuona mtoto anakaa chini, tunajaribu kuona kwamba kila kijiji kufikia mwaka 2025 kina Zahanati, haya ni malengo makubwa” alisema Spika Ndugai kwa uchungu.

Akiongelea ufikiaji wa malengo hayo makubwa ifikapo mwaka 2025, alisema kuwa utekelezaji wa sheria hiyo ni muhimu. “Tunayafikiaje malengo haya… ndio maana sisi wabunge tukaamua kwamba tunakwenda kwenye miamala, hasa ukinuna sawa ukifanyaje sawa, tunakwenda kwenye miamala. Tutatoza kakitu fulani (fedha kidogo) kwenye miamala, fedha inayopatikana sio kodi ya kawaida, inakwenda katika mfuko maalumu na fedha ile itarudishiwa wananchi wenyewe kupitia hayo maji, umeme, barabara za vijijini zote, madaraja, afya na kadharika, kupitia hii tozo ndogo ndogo ya kwenye miamala” alisisitiza Spika huyo.

Akiongelea sheria hiyo ya miamala, alisema kuwa, imetungwa na wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi. “Tumepitisha sisi, tukatunga sheria sisi, tunataka kuliona hilo, hakuna atakaekuja kutujengea nchi hii (amesema Profesa hapa). Unaepinga hilo sawa, tupe mbadala tunawezaje kuyafanya haya ifikapo 2025? Tutapata wapi fedha?... inawezekana kiwango ni kikubwa inatakiwa iwe kidogo kidogo hilo lina mjadala wake. Lakini lazima tufanye, kama tunavyofanya kwenye mambo mengi… mtu wetu wa kijijini awe kwenye darasa zuri lenye ‘tiles’ kama mtu wa mjini, apate huduma ya afya kama mtu mwingine yeyote. Kwa hiyo maamuzi haya tumeyafanya kwa nia njema kabisa kwamba mwaka 2025 tuwe ni taifa la Tanzania ambalo ni tofauti Afrika nzima” alisema Spika Ndugai.

Kikao kazi hicho kilihudhuriwa na wajumbe takribani 600 ikijumuisha Spika wa Bunge, Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa, Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (Mkoa na Wilaya), Kamati ya Usalama (Mkoa na Wilaya), Wabunge, wakuu wa Wilaya, Mstahiki Meya wa Jiji, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa. Wengine ni Wajumbe wa Timu ya Menejimenti ya Mkoa, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakuu wa Taasisi mbalimbali, Madiwani wa Halmashauri zote, Wajumbe wa Timu za Menejimenti wa Halmashauri zote na Waandishi wa Habari.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.