• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TAMISEMI yatoa vyeti kwa Mkurugenzi, walimu Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: August 4th, 2020

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi amepewa zawadi ya cheti na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kufuatia ubunifu wake wa kuanzisha program ya kufundisha wanafunzi kwa njia ya redio za Dodoma na mitandao ya kijamii katika mapumziko ya Covid-19.

Zawadi hiyo ya cheti imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Selemani Jafo katika siku ya TAMISEMI, maalum kwa sekta ya elimu iliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Dodoma leo.

Akitoa maelezo mafupi ya utangulizi kuhusu zawadi hivyo, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI anayeshughulikia elimu, Gerald Mweli amesema kuwa vyeti hivyo vinatolewa kwa watumishi waliofanya vizuri katika mapambano ya Covid-19 katika sekta ya elimu.

Vyeti hivi ni maalum kwa walimu wa Jiji la Dodoma kwa sababu wakati nchi inaendesha program ya kufundisha wanafunzi katika televisheni kitaifa, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi aliamua kuanzisha program yake katika redio za ndani ya Jiji la Dodoma kwa kutumia walimu wake. Hivyo, tukaona ni vema kuwatambua hii ni kutokana na maelekezo yako wewe mwenyewe mheshimiwa Waziri kuwa tuwatambue wale wote walioshiriki katika kufundisha wanafunzi wakati wa likizo ya Covid-19. Hivyo, hii ni zawadi maalum kwa Mkurugenzi wa Jiji na walimu wake” amesema Mweli.

Wengine waliopata zawadi za vyeti ni Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Joseph Mabeyo, Afisa Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma Upendo Rweyemamu na walimu wote walishiriki kufundisha vipindi katika redio za Jiji la Dodoma.

Akiongelea zawadi ya cheti hicho, mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma aliyepokea cheti hicho, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Sharifa Nabalang’anya amesema kuwa cheti hicho ni heshima kubwa kwa Halmashauri. “Mkurugenzi amepatiwa cheti hicho kwa kutambua juhudi za utoaji elimu kwa wanafunzi wakati wa mapambano ya Covid-19. Jiji liliona ni muhimu kwa wanafunzi kupata elimu kupitia redio na mitandao ya kijamii badala ya kubaki nyumbani. Cheti hiki ni heshima kubwa kwa Mkurugenzi wa Jiji na Halmashauri kwa ujumla” amesema Nabalang’anya.

Siku maalum ya TAMISEMI (TAMISEMI Day) kuhusu sekta ya elimu inalenga kuelezea mafanikio yaliyopatikana katika sekta hiyo na imehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Selemani Jafo.

Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Seleman Jafo (wa tatu kulia) akimkabidhi Sharifa Nabalang'anya aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kupokea cheti cha kutambua mchango wake wa kutoa elimu kwa wanafunzi wakati likizo ya mapumziko wakati wa mapambano ya Corona. Kulia kwa Waziri ni Katibu Mkuu wa OR-TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga.   

Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Upendo Rweyemamu (kushoto) akiwa na Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi Joseph Mabeyo wote wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma waliposhiriki kwenye Siku ya TAMISEMI (Sekta ya Elimu) ambapo walikuwa miongoni mwa waliotunukiwa Cheti kutambua mchango wao wa kutoa elimu wakati wa likizo ya Corona.


Baadhi ya walimu  kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma walioshiriki kutoa elimu kwa njia ya redio na mitandao ya kijamii wakati wa likizo ya Covid-19 ambao nao OR-TAMISEMI imewapa cheti kutambua mchango wao kwa jamii katika kutoa elimu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.