• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TANROADS, TARURA waagizwa kuwabana wakandarasi

Imewekwa tarehe: March 18th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge amewataka wataalamu wa Wakala wa barabara nchini TANROADS Mkoa wa Dodoma na Wakala wa barabara za mijini na vijijini TARURA kujenga utaratibu wa kuwa karibu na wakandarasi waliopewa miradi katika maeneo yao ili miradi hiyo itekelezwe kwa viwango na kwa wakati.

Dkt Mahenge ametoa maagizo hayo Machi 17, 2021 jijini Dodoma wakati wa kikao cha bodi ya barabara Mkoa wa Dodoma waliokutana kutathmini utekelezaji wa bajeti na namna ya kuboresha bajeti mpya 2021 hadi 2022 amesema kila taasisi katika eneo ambayo mkandarasi amesaini mkataba asimamiwe kikamilifu.

“Mimi nimepita katika miradi hiyo nimeona wakandarasi wapo site (eneo la kazi) na maeneo mengi wametengeneza lakini mvua zimeharibu na ukizingatia serikali imeshatoa fedha hakuna fedha nyingine mkandarasi asimamiwe akarabati kwenye uharibifu” amesema Dkt Mahenge.

Amesema taasisi hizo ni muhimu sana katika kuunganisha Mikoa, Wilaya, Vijiji na mitaa hivyo ni vyema viongozi wa taasisi hizo kufanyakazi kwa weredi kuhakikisha wananchi wanaunganishwa na mawasiliano ya barabara ili kujikwamua kiuchumi.

Aidha ameitaka TARURA kujenga utaratibu wa kutembelea halmashauri husika kabla ya kutenga bajeti au kuainisha barabara za kukarabati ili wapate mahitaji halisi kutoa kwenye halmashauri husika na uhitaji na umuhimu wa barabara kabla ya kuzitengea bajeti barabara hizo.

“TARURA muende kwenye halmashauri husika huko mtajua mahitaji halisi ya halmashauri hizo wao watawaambia bara bara ipi ni muhimu sana kwa kipindi hicho kuliko ninyi kupanga tu bajeti bila kujua sehemu zenye mahitaji sana” amesema.

Ametaka ahadi zote za viongozi wa kitaifa ziainishwe kwa Pamoja na zipewe kipaombele na msukumo ili fedha hizo ziweze kutengwa ili ahadi hizo zitimizwe, huku akiwataka viongozi wa ngazi zote katika halmashauri za Mkoa wa Dodoma kuwa wasimamizi wa miradi yote inayotekelezwa katika maeneo yao.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Wakala wa barabara nchini TANROADS Mkoa wa Dodoma Mhandisi Salome Kabunda akieleza utekelezaji wa miradi ya TANROADS amesema kwa mwaka wa fedha 2019 – 2020 walitengewa zaidi ya bilioni 18 kwa matengenezo na ukarabati wa barabara mbalimbali.

Amesema kwa mwaka wa fedha 2020 na 2021 pia walitengewa zaidi ya shilingi bilioni 18 kwa matengezezo ya barabara kuu na barabara za Mkoa huku ikiwa imesaini jumla ya miradi 37 ya barabara ikiwa na ujenzi wa madaraja makubwa mbalimbali.

Nae mratibu wa RARURA Mkoa wa Dodoma Mhandisi Lusako Kilembe amesema TARURA inajumla ya barabara zenye urefu wa kilomita 6996.25 kati ya hizo barabara 2695.75 barabara za mikusanyiko, 3403 barabara za mlisho na barabara 897 ni barabara za kijamii.

Akizungumza kwenye kikao hicho Katibu tawala Mkoa wa Dodoma Maduka Kessy amesema ni vyema wajumbe wa kikao hicho kushiriki katika vikao vya ngazi ya chini kwenye maeneo yao ili kubainisha changamoto na makubaliano tangu ngazi za chini katika maeneo wanayotoka.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.