• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tanzania ina chakula cha kutosha - Dkt. Mpango

Imewekwa tarehe: January 2nd, 2020

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema tatizo la ongezeko la bei la mazao kadhaa ni la muda, kwani hadi sasa nchi ina akiba ya chakula cha kutosha cha tani 53,000 katika kipindi cha mwaka 2019.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini hapa kuhusu Hali ya Uchumi kwa mwaka 2019, Dk Mpango alisema ongezeko la bei za bidhaa za vyakula, linategemewa kuwa la muda mfupi, kwani bado nchi inayo akiba ya kutosha ya chakula.

Alisema katika kipindi hicho, pia mfumuko wa bei wa chakula, uliongezeka kufikia wastani wa asilimia 6.7 Novemba 2019, ikilinganishwa na asilimia 2.0 katika kipindi kama hicho mwaka 2018.

Dk Mpango alisema ongezeko hilo, lilitokana na changamoto za usafirishaji, miundombinu ya masoko, maghala na ugavi wa bidhaa za vyakula kimaeneo. Alisema uhaba wa vyakula kwa nchi za jirani, ulisababisha soko la vyakula kwa nchi hizo kuwa kubwa na kuvutia wafanyabiashara nchini, kusafirisha bidhaa za chakula na kuziuza katika nchi hizo.

Dk Mpango alisema mfumuko wa bei, uliendelea kubakia ndani ya lengo la asilimia 5.0 katika mwaka ulioishia Novemba 2019. “Katika kipindi hicho, mfumuko wa bei ulifikia wastani wa asilimia 3.8 ukilinganishwa na asilimia 3.0 katika kipindi kama hicho 2018. Kiwango hiki ni chini ya lengo la nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki la asilimia 8,” alisema.

Alisema nchi nyingi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), nazo zilikuwa na viwango vidogo vya mfumuko wa bei. Dk Mpango alisema mfumuko wa bei katika kipindi kilichoishia Novemba 2019, kwa Kenya ni asilimia 5.6 na Uganda ilikuwa asilimia 3.

Alisema mfumuko wa bei wa chakula uliongezeka Novemba 2019, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2018 na ulitokana na changamoto za usafirishaji. “Ongezeko hili lilitokana na changamoto za usafirishaji, miundombinu ya masoko, maghala na ugavi wa bidhaa za vyakula kimaeneo,” alisema.

Chanzo: habarileo.co.tz



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.