• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Tanzania na Afrika kwa ujumla tunaweza" - JPM

Imewekwa tarehe: July 26th, 2019

*YALIYOJIRI WAKATI WA UWEKAJI JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA UZALISHAJI UMEME  KATIKA MTO RUFIJI*

*Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli*

#Siku hii ni ya kipekee sana kwa nchi yetu ikiwa tumeanza kutekeleza mradi huu wa ndoto ya mwalimu Nyerere kwani aliamini ni kichocheo cha ukuaji wa sekta zote.

#Kuja kwa wawakilishi kutoka Misri kwa ajili ya kushuhudia tukio hili ni ishara ya uhusiano mzuri uliopo baina ya nchi zetu hizi mbili.

#Ujengaji wa Uchumi wa viwanda kokote duniani ni lazima uwe na uhakika wa umeme na wa bei nafuu, mradi huu ni suluhisho.

#Nchi yetu imeudhihirishia ulimwengu kuwa sisi ni taifa huru na sio masikini, mradi huu ulipigwa vita ndani na nje ya nchi, sasa tunautekeleza kwa pesa zetu wenyewe.

#Mradi huu ni ishara kuwa Tanzania na Afrika kwa ujumla tunaweza.

#Mradi huu utazalisha umeme mwingi ambao ni mwingi kuliko umeme wote uliozalishwa nchini Tangu tumepata uhuru, tutakuwa na umeme wa kutosha, wa uhakika na wa bei nafuu.

#Mradi huu utasaidia kukuza sekta ya Biashara na uwekezaji nchini hasa kutokana na kuwepo kwa umeme wa uhakika na wa bei nafuu.

#Uwepo wa mradi huu utachochea fursa za Kilimo, Umwagiliaji na Uvuvi kwa wananchi wanaozunguka maeneo ya mradi.

#Utekelezaji wa Mradi huu pia utasaidia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa sekta ya utalii, wanyama wengi watakuja maeneo haya kunywa maji, utalii wa michezo na wale watakaokwenda kuangalia mitambo ya kuzalishia umeme.

#Ninaagiza kuwa sehemu ya Selous Game Reserve ikatwe na iwe Hifadhi ya Taifa.

#Ninaagiza barabara kutoka Eneo la Fuga mpaka eneo la Mradi ijengwe barabara kwa kiwango cha lami, na tutatumia fedha zilizorudishwa na ndugu yetu Mhe. Rais Uhuru Kenyatta.

#Niwapongeze wote wanaosimamia sekta ya nishati hasa TANESCO na Wizara ya Nishati, mnafanya kazi kubwa sana, hata mgao kwa sasa umepungua kwa kiasi kikubwa.

#Mpaka sasa tumepeleka umeme kwenye vijiji 7,419 ambapo ni ongezo la asilimia 254.

#Naombeni sana mkamilishe mradi huu kwa wakati na hata ikiwezekana kabla ya wakati, kwetu sisi pesa sio tatizo.

#Bima ya Mradi huu 100% lazima itolewe na Serikali, Waziri ulizingatie, Wizara ya Fedha mlizingatie, TANESCO mlizingatie, ole wenu mkatafute akasaini bima mtu binafsi.

#Wakazi wanaoishi maeneo haya ndio wawe kipaumbele katika kupatiwa ajira.

#Niwaombe wale wote watakaofanikiwa kupata kazi katika mradi huu, muwe waaminifu, msiibe chochote ili tuukamilishe kwa wakati na kwa ufanisi.

#Bwawa hili likikamilika liitwe BWAWA LA NYERERE, na hata sehemu ya Selous Game Reserve itakayokatwa iitwe NYERERE NATIONAL PARK.

*Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa*

#Ndoto yako leo Mheshimiwa Rais  ya kupeleka umeme kwa kila nyumba ya mtanzania mijini na vijijini inakwenda kutimia.

#Watanzania endeleni kuiunga mkono Serikali hii iendelee kuchapa kazi ili kuiletea maendeleo nchi yetu.

*Naibu Spika wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson*

#Sisi kama wawakilishi wa wananchi Bungeni tunakupongeza sana kwa kufanikisha utekelezaji wa mradi huu.

*Waziri wa Nishati wa Tanzania Dkt. Medard Kalemani*

#Nakupongeza kwa kutekeleza mradi huu, nina kuahidi kuusimamia, huu ni mradi kwa kwanza kusimamiwa na watanzania.

# Umeme huu utasafirishwa kutoka Rufiji kwenda Chalinze, Dar halafu Dodoma na ndio umeme utakaotumika katika kuendesha Treni ya Mwendokasi.

#Mradi huu ni moja ya utekelezaji wa ahadi kwa nchi kuzalisha Megawati 10,000 kufikia mwaka 2025.

#Mradi huu ni chachu katika kuendeleza sekta ya viwanda nchini.

*Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohammed Shakkah*

#Mradi huu unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya TANESCO na makampuni mawili ya Misri ni moja ya hatua kubwa ya mahusiano kati ya Tanzania na Misri.

#Mradi huu utasaidia Tanzania kuzalisha umeme wa kutosha na kutekeleza Malengo ya Milenia ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa.

#Mradi huu utawezesha Nchi ya Tanzania kuzalisha umeme wa kutosha na hata kuwa na uwezo wa kuzisaidia nchi jirani.

#Misri tutatoa nafasi 50 za mafunzo kwenye sekta ya Nishati kwa Watanzania.

*Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Dkt. Tito Mwinuka*

#Gharama ya Mradi huu ni Tsh Tril. 6.5 na mpaka sasa tumeshalipa 15% ya gharama hiyo ambayo ni TSh Tril 1.007.

#Mhe. Rais tunao umeme unaojitosheleza lakini kukamilika kwa mradi huu kutatuongezea ziada ya umeme utakaotusaidia kutekeleza kwa vitendo azma ya nchi kuelekea uchumi wa kati.

*Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Steven Kebwe*

#Mheshimiwa  Rais  nakupongeza kwa kutimiza ndoto hii ya Baba wa Taifa.

*Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo*

#Utekelezaji wa mradi huu ni moja ya suluhisho ya mafuriko yaliyokuwa yanatokea mara kwa mara kutokana na kufurika kwa Bonde la mto Rufiji.

#Tangu kuanza kutekelezwa kwa mradi huu, wananchi takribani 558 wameajiriwa kutoka maeneo ya Rufiji na Kibiti.

#Kutekelezwa kwa Mradi huu ni chachu ya kukua na kuendelea kwa sekta ya uwekezaji katika Mkoa wetu.

#Tumejipanga kuanza kilimo cha Michikichi, Mpunga na Miwa kutokana na kutekelezwa kwa mradi huu.

Chanzo: Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa ya Ikulu: Taarifa ya Ikulu: Dkt. John Magufuli aweka jiwe la msingi mradi wa kuzalisha umeme katika Mto Rufiji

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.