• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tanzania sasa inaongoza Afrika katika Hifadhi za taifa

Imewekwa tarehe: September 11th, 2019

Bunge jana lilikubali kuunda mbuga tatu za kitaifa, na kufanya idadi ya mbuga nchini kufikia 24 ambayo ni idadi ya juu zaidi barani Afrika.

Akizungumza baada ya kuidhinishwa kwa mpango huo, Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla aliielezea hatua hiyo kama hatua muhimu katika azma ya Tanzania ya kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini kila mwaka.

Hifadhi mpya za kitaifa  zinatokana na kupandishwa hadhi kwa pori la akiba la sasa la Kigosi katika Mkoa wa Kigoma na pia pori la akiba Ugalla lililopo karibu na Mkoa wa Tabora.

Hifadhi hizo tatu zitaongeza idadi ya mbuga za kitaifa kutoka mbuga 19 za ardhi zinazosimamiwa sasa na Hifadhi za Kitaifa za Tanzania (TANAPA) hadi kufikia 22 pamoja na mbuga mbili mbili za baharini ambazo ni Hifadhi ya Marine Island kwenye ukanda wa pwani na Mnazi Bay-Ruvuma Estuary Marine Park.

"Kwa hesabu ya mbuga hizo 24 za kitaifa nchi yetu itaongoza bara la Afrika kwa idadi kubwa zaidi ya hifadhi za kitaifa, ikiipita Kenya ambayo ina hifadhi 23" alisema Dk Kigwangalla.

Waziri huyo alionyesha matumaini kwamba kwa kuongoza katika idadi ya mbuga za kitaifa, Tanzania itakuwa kwenye nafasi nzuri kuliko ilivyokuwa hapo awali katika juhudi zake za kuongeza utalii wa kimataifa pamoja na kupata fedha nyingi za kigeni zinazohitajika sana kukuza uchumi wetu.

"Hii inatupa fursa katika kuitangaza nchi kama sehemu yenye idadi kubwa ya vivutio vya utalii" alisema.

Hata hivyo, wakichangia hapo awali, baadhi ya Wabunge walitahadharisha kwamba kuna maswala ambayo yanapaswa kutafutiwa ufumbuzi kabla ya kuendelea na mpango huo.

Akiwasilisha mapendekezo ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mwenyekiti Kemilembe Lwota alisema kwamba ili kuhakikisha tunazuia mizozo kuhusu mbuga mpya za kitaifa, serikali inapaswa kufanya kazi na jamii zinazoishi ndani au karibu na maeneo yaliyotengwa ili kuhakiki mipaka.

"Kuna vijiji vinavyotambuliwa kisheria ndani ya mbuga. Kuna watu wengi wanaojihusisha na shughuli za ufugaji wa nyuki ndani ya mbuga zote mbili na pia idadi kubwa ya watu ambao maisha yao yanategemea uvuvi kwenye Mto Ugalla" alisema Lwota.

Mnamo mwezi Julai, Rais John Magufuli alitoa agizo la kuanzishwa kwa Hifadhi ya Kitaifa ya Nyerere, ambayo itamegwa katika sehemu ya juu ya Hifadhi ya Mbuga ya Selous.

Kabla ya agizo hilo, Rais alikuwa aliagiza Hifadhi ya Kitaifa ya Burigi-Chato ambayo ilipandishwa kutoka hadhi ya pori la akiba.


Chanzo: Gazeti la The Guardian (www.ippmedia.com)



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.