• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tanzania, Uganda kuunganisha Mkongo wa Mawasiliano

Imewekwa tarehe: September 29th, 2023

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amesema kiasi cha Bilion 71.7 za Kitanzania zitatumika kuiunganisha Uganda na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa kipindi cha miaka 15.

Waziri Nape ameyasema hayo wakati wa Hafla ya Utiaji Saini Makubaliano ya Kibiashara ya Kuunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) na Miundombinu ya Mkongo wa Taifa  wa Uganda (NBI) iliyofanyika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam, leo Septemba 29, 2023.

“Leo hii tumeshuhudia utiaji saini wa Mkataba wa kuunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano – NICTBB na Mkongo wa Mawasiliano wa Uganda. Mkataba huu una thamani ya kiasi cha Dola za Kimarekani Milioni 28 sawa na fedha za Kitanzania Shilingi Bilion 71.7 kwa kipindi cha miaka 15. Mikongo hii itaunganishwa kupitia mpaka wa Tanzania na Uganda, eneo la Mutukula katika Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera.” Amesema Waziri Nape.

“Ni matumaini yetu, kuona Afrika ya Kidigitali (Africa Digital) inafikiwa na matokeo yake chanya yanasaidia katika kuongeza kasi ya kukua kwa uchumi na shughuli za kijamii barani Afrika kwa kutumia teknolojia. Ni matumani yetu kuona Afrika yenye mifumo imara ya Serikali Mtandao, Elimu Mtandao, Afya Mtandao, Biashara Mtandao, Kilimo Mtandao katika kutoa huduma kwa wananchi wetu.” Amesema Waziri Nape.

Aidha, Waziri Nape ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika kusimamia vyema kutoa huduma kwa mujibu masharti yaliyopo kwenye mkataba wa makubaliano.

“Tuhakikishe tunatoa huduma bora na yenye uhakika, panapotokea changamoto yoyote ile iweze kushughulikiwa kwa haraka. Uganda inategemea huduma bora kutoka kwenu, mkatoe huduma yenye ubora kwa kuzingatia makubaliano ya Waheshimiwa Ma-Rais wetu. Kwa changamoto ambazo zitakuwa nje ya uwezo wenu, mziwasilishe Wizarani kupata ufumbuzi wa haraka”. Amesisitiza Waziri Nape.

Katika hatua nyingine, Waziri Nape amelipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania, Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Peter Ulanga na Dkt. Hatwib Mugasa Mkurugenzi Mtendaji wa NITA-U kwa kubeba jambo hili kwa uzito wake na kufanikisha kuunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano wa Tanzania –NICTBB na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano wa Uganda unaosimamiwa na NITA-U.

Mkataba huo umekuja mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipofanya ziara ya kikazi nchini Uganda, ambapo yeye na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoel Kaguta Museveni walikubaliana kuunganisha miundombinu mikuu ya mawasiliano ili kuiwezesha Uganda na nchi jirani kupata huduma za intaneti zenye ubora na bei nafuu na pia kuunganisha nchi ya Uganda na mikongo ya baharini iliyopo Tanzania.

Mkurugenzi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (kushoto), Mhandisi Peter Ulanga akiwa pamoja na Dkt. Hatwib Mugasa, Mkurugenzi Mtendaji wa NITA-U wakisaini Makubaliano ya Kibiashara ya Kuunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) na Miundombinu ya Mkongo wa Taifa  wa Uganda (NBI) hafla iliyofanyika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam, leo Septemba 29, 2023.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.