• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tanzania yang’ara ubunifu wa kiuchumi duniani

Imewekwa tarehe: September 4th, 2020

TANZANIA imepanda kwa nafasi tisa kutoka kutoka ya 97 hadi ya 88 duniani huku ikishika nafasi ya pili kwa nchi za Afrika Mashariki.

Vilevile imeshika nafasi ya tatu katika nchi za kusini ya jangwa la Sahara. Nchi hii imepanda hadi nafasi ya tisa ikilinganishwa na ripoti kama hiyo mwaka jana.

Katika ripoti ya jarida la Global Innovation Index ya mwaka huu, lililofanya utafiti Julai mwaka jana hadi Juni, mwaka huu kabla ya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati, nchi hii imepanda hadi nafasi ya tisa ikilinganishwa na ripoti kama hiyo mwaka jana.

Jarida hilo la Global Innovation Index hutolewa na World Intellectual Property Organization, WIPO.

Pamoja na hayo, kwa mujibu wa ripoti hiyo, Tanzania imeshika nafasi ya tatu katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara na pili katika nchi za Afrika Mashariki ikitanguliwa na Kenya.

Kenya mwaka huu, imeshika nafasi ya 10 katika nchi zenye uchumi wa kati ikishika nafasi ya 86 kati ya nchi 131 zilizofanyiwa utafiti duniani.

Ripoti hiyo inaonesha kuwa katika nchi hizo za uchumi wa chini, Tanzania imeshika nafasi ya kwanza ikifuatiwa na nchi za Rwanda iliyoshika nafasi ya pili na Nepal iliyoshika nafasi ya tatu.

Kwa nchi za Afrika Mashariki, pamoja na Kenya iliyoshika nafasi ya 86, Rwanda ilishika nafasi ya 91 na Uganda nafasi ya 114. Kwa kuzingatia nafasi hizo Tanzania ni ya pili Afrika Mashariki kwa ubunifu.

Aidha, kwa mujibu wa ripoti hiyo kwenye nchi za Jangwa la Sahara, Tanzania ilishika nafasi ya tatu kwa ubunifu wa kiuchumi, ikitanguliwa na Afrika Kusini iliyoshika nafasi ya kwanza na Kenya iliyoshika nafasi ya pili.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo inayotolewa kila mwaka ikiangalia ubunifu wa nchi katika kukuza uchumi, mwaka huu Tanzania imeingia pia katika nchi 41 ambazo maendeleo yake yako kiwango cha juu cha matarajio ya utafiti huo.

Historia ya ripoti hizo kwa miaka mitatu zinaonesha nchi hiyo imekuwa ikipanda na kushuka katika eneo la ubunifu wa uchumi ambapo mwaka 2017 ilishika nafasi ya 96, mwaka 2018 nafasi ya 92, mwaka jana nafasi ya 97 na mwaka huu imeshika nafasi ya 88 kati ya nchi 131 zilizofanyiwa utafiti.

Aidha, ripoti hiyo ya Global Innovation Index ya mwaka huu, ilieleza kuwa maeneo yaliyopimwa kwa ubunifu katika nchi hizo 131 ikiwemo Tanzania ni ubunifu katika miundombinu, mapato katika maarifa na teknolojia, mitaji ya binadamu na utafiti.

Maeneo mengine ni matokeo ya ubunifu, taasisi, uboreshaji wa biashara, uboreshaji wa masoko ambayo tangu mwaka jana ripoti hiyo imeonesha kuwa Tanzania inayatekeleza vizuri kiubunifu.

Pamoja na hayo, katika ripoti hiyo ya mwaka huu, imeitaja Uswizi kuwa nchi ya kwanza duniani kwa ubunifu ikifuatiwa na Sweden na Marekani. Huku nchi tatu za mwisho kwa ubunifu ni Yemen, Guinea na Myanmar.

Chanzo: HabariLeo


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.