• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tanzania yaongoza ukuaji uchumi EAC wakati wa Corona - AfDB

Imewekwa tarehe: September 16th, 2020

TANZANIA imeongoza kwa ukuaji mzuri wa uchumi katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na eneo zima la Mashariki mwa Afrika lenye nchi 13, katika kipindi chote cha janga la virusi vya corona.

Hayo yamebainishwa katika Ripoti ya Uchumi wa Afrika ya 2020 ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ambayo imetoa tathmini ya athari za virusi vya corona katika kanda tano za Bara la Afrika, ambapo Kanda ya Mashariki ndiyo iliyofanya vizuri zaidi kiuchumi.

Kanda zilizoainishwa katika ripoti hiyo na ukuaji kiuchumi katika mabano ni Kanda ya Mashariki mwa Afrika yenye nchi 13 (0.9), Afrika Magharibi yenye nchi 16 (-2.0), Kaskazini mwa Afrika yenye nchi sita (-0.8), Afrika ya Kati yenye nchi nane (-2.5) na Kusini mwa Afrika yenye nchi 14 (-4.9).

Katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kipindi cha virusi vya corona, Tanzania imeongoza katika makadirio ya ukuaji wa uchumi kwa kuwa na wastani wa asilimia 5.2, ikifuatiwa na Rwanda (4.2), Uganda (2.5), Kenya (1.4), Sudan Kusini (-0.4) na Burundi (-5.2).

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mambo yaliyosababisha Afrika Mashariki na eneo zima la Mashariki mwa Afrika kufanya vizuri kiuchumi kuliko kanda zote barani Afrika ni pamoja na matumizi makubwa katika miundombinu, kupanda kwa mahitaji ya ndani, kuimarika kwa hali ya usalama, kuwapo kwa fursa mpya za uwekezaji na misamaha katika kuchochea ukuaji wa viwanda.

Ripoti hiyo imeeleza kuwa Tanzania imefanikiwa kukuza kiuchumi wakati wa kipindi cha corona kutokana na hatua ilizochukuwa kukabiliana na maambukizi ya virusi hivyo bila kuathiri shughuli za kiuchumi na biashara, wakati nchi zilizochukua hatua kali, uchumi wake umeporomoka.

Sababu zilizotajwa za baadhi ya nchi kuporomoka kiuchumi ni kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo ziligeuzwa matumizi na kutumika katika kupambana na virusi hivyo.

Sababu nyingine ni kudorora kwa ukusanyaji wa mapato hasa kwa nchi zilizoweka na kutekeleza sheria ya kukaa ndani ‘lock down’ kama vile Kenya, Uganda, Sudan Kusini na Rwanda.

Ripoti hiyo ilisema ukusanyaji wa mapato katika nchi hizo, ulikuwa mdogo kwa kuwa biashara nyingi zilifungwa kwa ajili ya kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona.

Katika nchi za Afrika Mashariki, Tanzania ndio taifa la kwanza kufungua milango ya kiuchumi na kutoweka sheria ya ‘lock down’, hali inayotajwa na ripoti hiyo kuwa yenye manufaa makubwa kwa uchumi wake na kanda nzima ya Afrika Mashariki.

Sababu nyingine iliyosababisha Tanzania kufanya vizuri katika kipindi hicho ni kuitikia kiu ya soko la kimataifa.

Pamoja na sheria ya ‘lockdown’ katika mataifa mengi duniani, usafirishaji wa mizigo uliendelea na Tanzania ilitumia mwanya huo kusafirisha bidhaa zake katika masoko mbalimbali kimataifa.

Pia Tanzania imetajwa katika ripoti hiyo kuwa imefanikiwa kutengeneza ajira nyingi zaidi kuliko nchi nyingine za Afrika Mashariki.


Chanzo: HabariLeo

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.