• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TEA, Jiji la Dodoma kutumia bilioni 1.9 kukarabati shule

Imewekwa tarehe: May 7th, 2021

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeendeleza jitihada katika kukuza sekta ya elimu kwa kuboresha miundombinu na upanuzi wa shule Jijini hapa ikishirikiana na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) pamoja na taasisi nyingine za kifedha nchini.

TEA na Halmashauri ya Jiji la Dodoma zimrfanya hafla ya makabidhiano rasmi ya mradi wa ukarabati na upanuzi wa shule za msingi Kisasa, Kizota, Medeli na Mlimwa C jana tarehe Mei 6, 2021 ambapo mradi huo unafanyika chini ya mshauri elekezi Chuo cha Sayansi Mbeya (MUST Consultancy Bereau - MCB) wenye gharama ya shilingi Bilioni 1.9 na unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi minne kutoka sasa.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, iliyofanyika katika shule ya msingi Mlimwa C, Prof. Davis Mwamfupe amesema kuwa dhana ya Makao Makuu ina uwanda mpana na kuijenga inahitaji taasisi zote kushirikiana na kwamba suala la kutoa pesa ni jambo moja, kuzipokea na kuzielekeza katika matumizi sahihi ni jambo jingine la wa pili.

“Nakuagiza Mkurugenzi hatutegemei ucheleweshwaji wowote katika kutekeleza mradi huu, kucheleweshwa ni kuruhusu kukauka kwa zege, ucheleweshwaji ambao hauna maelezo hatutaukubali na kamati yangu ya fedha tunataka taarifa ya maendeleo ya mradi huu” alisema Prof. Mwamfupe.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa TEA Bahati Geuzye alisema kuwa, taasisi hiyo ya Serikali ambayo inafanya kazi chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambayo ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 8 ya Mfuko wa Elimu ya mwaka 2001 ikiwa na jukumu la kusimamia na kuratibu mfuko wa Elimu.

“Mamlaka inaanza rasmi utekelezaji wa mradi wa kuboresha miundombinu ya Elimu katika shule nne za msingi Jijini Dodoma kwa lengo la kusaidia jitihada za Serikali katika kuboresha sekta ya Elimu, mradi huu ni miongoni mwa miradi 123 kwa mwaka wa fedha 2019/ 2020 ila ulichelewa kutokana na changamoto kadhaa lakini kwa sasa tumepata ufumbuzi na mradi unaenda kutekelezwa” alisema Geuzye.

Akizungumza kwa niaba ya walimu wakuu wa shule zitakafikiwa na mradi huo, Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Medeli Grace Lisasi alieleza kiasi gani mradi huo ulivyo na faida kwani katika shule yake umefanya ufaulu kuongezeka toka asilimia 57 na kufikia asilimia 82 kutokana na mradi wa awamu ya kwanza.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.