• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TEHAMA itaongeza uwezo wa utoaji elimu na ufaulu – Waziri Nape

Imewekwa tarehe: June 17th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

SERIKALI imesema kuwa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yatasaidia kuongeza uwezo wa utoaji elimu na kuongeza ufaulu kwa shule za sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya TEHAMA katika shule ya sekondari Chinangali iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma leo tarehe 16 Juni, 2022.

Waziri Nnauye alisema kuwa wizara yake kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) inakabidhi vifaa vya TEHAMA ili viweze kusaidia kuongeza uwezo wa utoaji elimu jijini hapa. “Ni matumaini yangu kuwa vifaa hivi vya TEHAMA vitaenda kuongeza uwezo wa utoaji elimu. Ufaulu utaongezeka, uelewa wa wanafunzi utaongezeka na uwezo wa kukabiliana na mazingira utaongezeka” amesema Waziri Nnauye.

Waziri huyo alitumia jukwaa hiyo kuiasa jamii juu ya madhara yatokanayo na matumizi ya TEHAMA yasiyo sahihi. Alisema kuwa TEHAMA ina uwezo wa kusambaa na tamaduni za kigeni zikamharibu mtoto wa kiafrika kutokana na matumizi ya mtandao wa ‘Internet’.

Aidha, aliwataka wazazi kuwalinda watoto ili wasiharibiwe na maendeleo na kasi ya ukuaji wa TEHAMA. “Wazazi tusiwazuie watoto kutumia TEHAMA ila tuwalinde dhidi ya madhara yake. Tuwaambie watoto ukweli ili wawe huru” alisema waziri Nnauye.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini, Mhe. Anthony Mavunde alisema kuwa siku hiyo ya mtoto wa Afrika ni ya kipekee. “Leo ni siku ya mtoto wa Afrika. Kipekee wananchi wa Dodoma tumepata heshima kubwa ya ugeni wako. Ni siku jamii inajikumbusha matukio yote yaliyompata mtoto. Tutahakikisha tunalinda na kusimamia watoto wetu ili wafikie malengo yao.

Aidha, alimshukuru Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kuiwezesha shule hiyo kupata kompyuta. Alisema kuwa mpango wake ni kuziwezesha shule zote za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupata kompyuta.

 Nae Afisa Elimu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alishukuru kuichagua shule hiyo kupata vifaa hivyo vya TEHAMA. “Ndugu mgeni rasmi, sisi tumefurahi sana. Tunashukuru sana kwa vifaa hivi, nikuhakikishie tutavitunza na mwakani vifaa hivi vitazaa matunda na kuongeza ufaulu” alisema Mwalimu Rweyemamu.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.