• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Teknolojia kutumika, fomu za uhiari wa kupata huduma ya chanjo dhidi ya Korona

Imewekwa tarehe: July 15th, 2021

MKURUGENZI wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Leonard Subi amesema kuwa Serikali imejipanga kuwa na mifumo miwili ya kujaza fomu ya uhiari wa kupata huduma ya chanjo ya Korona ikiwemo kupitia njia ya kielektroniki na njia ya karatasi.

Siku moja nyuma fomu ya kujaza kupata huduma ya kupata chanjo ilisambaa katika mitandao ya kijamii huku wananchi wengi wakihoji maswali mengi kuhusu utaratibu huo.

Hata hivyo Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Aifello Sichwale amesema fomu hiyo iliyotolewa katika mwongozo wa Serikali kuhusu chanjo ni ya kawaida na itakua inafafanuliwa vema kwa watakaohiari kupata chanjo na kuwasihi wananchi kupuuza taarifa za mitandaoni.

Dkt. Subi alizungumza leo Julai 15, 2021 ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu kwa wananchi juu ya mlipuko wa tatu wa ugonjwa wa Korona na umuhimu wa chanjo ili kupambana dhidi ya ugonjwa huo.

“Utaratibu ambao Serikali imeuweka tutakuwa na mifumo ya aina mbili moja itakuwa ni mfumo ya kielektroniki ambapo mtu anaweza akatoa uhiari wake kwa kujaza mwenyewe kwamba anahitaji kwenda katika kituo fulani kupata chanjo za ugonjwa wa Covid-19,” alisema Dkt. Subi.

Aliendelea kusema kuwa, Wizara ya Afya, imekuwa ikiendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma mbalimbali za tiba na kinga, hivyo kusisitiza kuwa baada ya utoaji wa elimu, mwananchi anakuwa na uhiari wa kupata huduma au kutopata.

“Tumekuwa tukiwapatia wananchi elimu ya kutosha juu ya huduma fulani, sasa ukishampatia elimu ya kutosha, mwananchi anakuwa na uhiari wa kupata huduma au kutoipata, sawasawa na mgonjwa anapoenda kufanyiwa huduma za upasuaji, tumekuwa tukimpatia huduma ya fomu ya uhiari,” amesema Dkt. Subi.

Aidha, Dkt. Subi amesema kuwa, hiari inaweza kuwa kwa njia ya mdomo au maandishi, hivyo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Korona Serikali ikaona ni vizuri kwa Watanzania kuendelea kutoa hiari yao katika kupata huduma hizo za chanjo ya Korona.

Mbali na hayo Dkt. Subi aliwatoa hofu wananchi kwa kusema kuwa, chanjo za ugonjwa wa Korona ni bora, salama, zina ufanisi wa kutosha na zimeorodheshwa na Shirika la Afya Duniani kwaajili ya matumizi ya dharura ili kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Korona.

“Chanjo hizi ni salama na zina ufanisi wa kutosha lakini pia ni bora, zimeorodheshwa na Shirika la Afya Duniani kwaajili ya matumizi ya dharura hususan katika kipindi hiki ambacho dunia imekumbwa na wimbi kubwa la ugonjwa wa Covid – 19,” amesema Dkt. Subi

Amesisitiza kuwa, Serikali imedhamiria kwa dhati kuutokomeza ugonjwa wa Korona na ndio maana inatumia afua zote za kupambana dhidi ya maambukizi ikiwemo uvaaji sahihi wa barakoa, kunawa mikono kwa sabuni na maji safi tiririka, kuepuka misongamano isiyo ya lazima, kutumia vipukusi, kufanya mazoezi na matumizi ya chanjo ya ugonjwa wa Korona.

Hata hivyo, Dkt. Subi amewatoa hofu Watanzania na kuwataka waendelee kuiamini Serikali na kufuata maelekezo yote kutoka kwa wataalamu wa afya katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo, huku akisisitiza kuwa sayansi haiwezi kupindishwa na maneno ya mitandao ya kijamii.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.