• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Timizeni wajibu wenu na kutatua migogoro kwa haki..." - Mkurugenzi Kunambi

Imewekwa tarehe: September 14th, 2019

WATENDAJI Kata na Mitaa na watumishi wa Idara ya Mipango miji, Ardhi na Maliasili katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutimiza majukumu yao kwa mujibu wa sheria ili waweze kutoa huduma bora kutatua migogoro ya ardhi inayowakabili wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi katika kikao cha kazi baina yake na watendaji hao katika ukumbi wa J.K. Nyerere wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini - Dodoma.

Kunambi alisema kuwa jukumu la msingi kwa watendaji wote ni kuwahudumia wananchi kwa viwango stahiki. “Watendaji wa Kata na Mitaa timizeni majukumu yenu. Mkumbuke kuwa mna kofia mbili, ya Mkuu wa Wilaya na ya Mkurugenzi wa Jiji. Hivyo, lazima matatizo ya wananchi yawaguse na muone mnawajibu katika kuyatatua. Mkiona wananchi wengi wanakuja kwenye ofisi zenu mjue kuna matumaini wanayoyapata kutoka katika ofisi zenu. Ila mkiona hawaji na wanakimbilia kwa Mkurugenzi mjue hamtimizi wajibu wenu” alisema Kunambi.  

Mkurugenzi aliwataka watendaji kufanya ukaguzi na kuzuia ujenzi holela katika maeneo yao.  Alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inajengwa katika karne ya 21 kwa kuzingatia taratibu za ujenzi na mipango miji. Kila ujenzi unatakiwa kufuata taratibu ikiwemo kupata kibali cha ujenzi ili kuepuka ujenzi holela. Aliwataka watendaji hao kuweka mpango wa kudhibiti ujenzi holela na kukagua uhalali wa vibali vya ujenzi katika maeneo yao yote.

Aidha, aliwataka watendaji kujiepusha na kuomba na kupokea rushwa katika utendaji wao wa kazi. Alisema kuwa sekta ya ardhi inalalamikiwa sana na wananchi na kuwa na migogoro mingi. “Migogoro mingi ya ardhi ni ya kurithi kutoka iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu. Na changamoto kubwa wananchi hawakuwa wakipata fursa ya kusikilizwa. Katika kutatua migogoro ya ardhi, Halmashauri ya Jiji imetoa viwanja mbadala na viwanja vya gharama nafuu zaidi ya 3,000 kwa wananchi. Hakuna eneo lolote nchini wananchi wamepewa viwanja bure, ni Dodoma pekee” alisema Kunambi.

Kikao kazi hicho kilihudhuriwa na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wakati chuo cha Serikali za Mitaa- Hombolo kiliwakilishwa na Mkufunzi aliyetoa mada kuhusu Wajibu na Majukumu ya Watendaji wa Kata/Mitaa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) walitoa mada kuhusu mbinu na mikakati ya kupambana dhidi ya rushwa.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.