• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Timu za kata ziwajengee uelewa wanavikundi – Mhe. Mwanyemba

Imewekwa tarehe: October 13th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeshauri kuundwa timu katika kila kata zitakayohusika kuvijengea uelewa vikundi vinavyokopeshwa viweze kurejesha mikopo kwa wakati ili wakopaji wengine waweze kunufaika.

Kauli hiyo ilitolewa na kiongozi wa timu namba moja ya wajumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mhe. Jaffar Mwanyemba alipoongea baada ya kutembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mhe. Mwanyemba alisema “tumeweza kufanikiwa kutembelea miradi sita ambayo ina uwiano tofauti. Tukichukulia vikundi vya watu wenye ulemavu na vijana waliokopeshwa ni kweli kwamba wamekopeshwa ila nadhani tunatakiwa tujiongeze. Huenda kwenye kata tuunde timu ambazo zitakuwa zinawapitia wanavikundi waliokopa, kuwakumbusha na kuwajengea ufahamu kuwa huo mkopo ni deni na wanatakiwa kurudisha ili fedha hizo ziweze kuwasaidia wao kukopa tena au wengine pia waweze kukopa” alisema Mwanyemba.

Aidha, aliwataka waliokopa kulipa kwa mujibu wa mikataba ya mikopo waliyokopa. “Waliokopa waende sambamba na maandishi yaliyowawezesha kuweza kupata mikopo yao. Tujaribu kuwasumbua sana vinginevyo tutakuwa na mpango mzuri wa serikali kuwakopesha ila hautakuwa na maana kwa sababu hauna matokeo mazuri. Matokeo yake, fedha ya serikali itakuwa inapotea na serikali itakuwa haina fedha nyingine za kuwakopesha wanavikundi wengine wenye uhitaji” alisema Mwanyemba.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Asha Vuai alisema kuwa wataalam wa wamepokea maelekezo na ushauri ya madiwani. “Leo tupo na ziara ya waheshimiwa madiwani wa Kamati ya Fedha na Utawala. Tumetembelea miradi mbalimbali ikiwemo vikundi vinavyonufaika na mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. Vikundi vinne vimetembelewa vya vijana viwili, kina mama kimoja na wenye ulemavu kimoja. Waheshimiwa madiwani wameshauri na wametoa maelekezo yao. Sisi kama wataalam tunaahidi tutayatekeleza kwa kuyafanyia kazi yale yote waliyoshauri” alisema Vuai.

Alisema kuwa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana inaendelea kuhamasisha vikundi ili viendelee kufanya marejesho kwa wakati. Vikundi vikifanya marejesho kwa wakati vinatoa fursa kwa vikundi vingine kuweza kukopeshwa, aliongeza.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.