• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Toeni taarifa kwa uongozi wa Kata, Mtaa au Ofisi za Halmashauri ya Jiji pindi wanaposhuhudia uchafuzi wa mazingira - Kimaro

Imewekwa tarehe: July 27th, 2023

WANANCHI wa Dodoma watakiwa kulinda mazingira na kutoa taarifa kwa uongozi wa Kata, Mtaa au Ofisi za Halmashauri ya Jiji pindi wanaposhuhudia mtu au watu wakifanya uchafuzi wa mazingira wa aina yoyote ili taratibu za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Wito huo ulitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi, Dickson Kimaro alipokua akiongea na waandishi wa habari.

Kimaro alisema kuwa swala la usafi ni ustaarabu na unatakiwa uanze na sisi wenyewe, kila mmoja awajibike kulinda mazingira kwa kuhakikisha mazingira yanayomzunguka ni safi “kumekuwa na tabia ya wafanyabiashara hasa wa maduka kufanya usafi kwenye maduka yao nakutupa uchafu kwenya mitaro ya maji ya mvua, pia wafanyabiashara wa chakula wamekua wakimwaga maji machafu kwenye mitaro hivyo,  kusababisha mitaro kuziba hasa kipindi cha mvua. Dodoma tuna kampeni ya ‘Mita tano usafi wangu usafi wangu mita tano’ nitoe wito kwa wananchi ukiona  mtu, mwenye duka, mwenye biashara au mwenye nyumba anafanya uchafuzi wa mazingira na kutupa taka hovyo kuzunguka eneo lako toa taarifa haraka kwenye Ofisi za Kata au Mtaa zilizopo karibu yako au tupigie simu ili tutume mgambo aende kumkamata kwaajili ya taratibu zingine za kisheria”.

Akiongelea hatua wanazozichukua kama jiji pindi wanapomkamata mharibifu  wa mazingira alisema kuwa tunapofanya ukaguzi wa siku kwa siku kupitia maafisa Afya, Mazingira na Polisi Jamii waliopo kwenye kata, wamekuwa wanawachukulia hatua  wakiwakamata waharifu kwa kuwatoza  faini ya kuanzia shilingi 50,000/= hadi 300,000/= kutegemeana na ukubwa wa tatizo alilosababisha kwenye uharibifu wa mazingira.

“Ingawa kumekuwa na baadhi ya wananchi wamekuwa wakiharibu mazingira kwa kutupa takataka kwenye mitaro ya maji ya mvua , wengine wamekuwa wakikusanya takataka  kwenye nyumba zao na kuchoma katikati ya mitaro licha ya jitihada tunazozifanya. Tumechukua hatua kubwa sana kwa mwaka wa fedha uliopita kwenye kipengele cha uchafuzi wa mazingira pekee  tumekusanya zaidi ya milioni 46 kupitia faini mbalimbali za uchafuzi wa mazingira” alisema Kimaro.

Alimalizia kwa kuwashauri wakazi wa Dodoma kuwa na kasumba ya kupenda usafi na kushiriki kwenye shughuli za usafi wa mazingira sababu wamepata dhamana kubwa sana yakuidhinishwa kuwa jiji hivyo, wanatakiwa kuwa jiji la mfano kwa kuhakikisha mazingira yao ni safi na salama.

“Niwaombe wakazi wa Dodoma kuwaunga mkono viongozi wa kata na mitaa ambao wanawajibu wa kusimamia usafi kwa kujitokeza kwa wingi kila Jumamosi kushiriki zoezi la usafi wa mazingira katika mitaa yenu. Kwa pamoja tunaweza kuyatunza mazingira yetu na kuifanya Dodoma kuwa jiji safi” alimalizia Kimaro.

Kwa upande wake Elia Nyoni, mkazi wa mtaa wa Kizota aliupongeza uongozi wa Jiji la Dodoma kwa kuhakikisha maeneo ya umma na wazi kama makaburi yapo safi “kusafisha maeneo kama hayo ni ibada kwa sababu tunasafisha na kuweka safi maeneo ambayo wenzetu wamelala. Sasahivi ukienda makaburi ya Kizota ni masafi nawapongeza sana kwa kuyapa kipaumbele maeneo ya umma kwenye usafi. Niwaombe wanadodoma wenzangu tuendelee kuwaunga mkono katika shughuli za usafi  na kutoa taarifa sehemu husika kwa wote wanaovunja sheria za mazingira” alisema Nyoni.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.