• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TPSF yaahidi kuunga mkono juhudi za Jiji Dodoma

Imewekwa tarehe: November 23rd, 2020

Taasisi ya sekta binafsi Tanzania imeahidi kuunga mkono Juhudi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma za kuvutia wawekezaji kuwekeza jijini hapo na kuzalisha ajira.

Ahadi hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya sekta binafsi Tanzania, Zachy Mbenna (pichani), alipokuwa akiongea katika mkutano wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania "Private sector breakfast meeting" uliofanyika katika hoteli ya Dar es salaam Serena mwishoni mwa wiki.

Mbenna alisema “agenda ya kuvutia wawekezaji Halmashauri ya Jiji la Dodoma tutaiweka kwenye agenda zetu za kudumu kutokana na hii heshima kubwa ambayo Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetupatia, tutakuwa mabalozi wazuri kwa kuvutia wawekezaji. Tunaamini kupitia nyie hakuna muwekezaji atakayeumizwa” alisema.

Aidha, aliahidi kuendelea kushirikiana na halmashauri hiyo katika kufanikisha agenda hiyo, pamoja na kuialika halmashauri hiyo katika mikutano mbalimbali itakayokuwa ikiendeshwa na taasisi hiyo.

Kwa upande wake, Mchumi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fred Robert wakati akiwasilisha mada juu ya fursa za uwekezaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, alisema kuwa Halmashauri hiyo imekamilisha Mpango Kabambe (Master Plan) ulioainisha fursa za uwekezaji katika Jiji hilo kwa lengo la kutoa huduma bora za kijamii, uwekezaji na kukuza uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.

“Mpango Kabambe wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma umeainisha maeneo ya uwekezaji katika nyanja za elimu, afya, biashara, kilimo, burudani pamoja na mengine” alisema Robert.

Akiongelea uwekezaji katika sekta mbalimbali, alizitaja kuwa ni elimu na kusema maeneo ya uwekezaji yapo katika ujenzi wa vyuo, shule na maeneo ya michezo. “Kwa upande wa Afya, maeneo yaliyopimwa yapo kwa ajili ya ujenzi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati. Vilevile, yapo maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanda, hoteli na maduka makubwa yaani shopping malls” alisema Robert.

Maeneo mengine ya uwekezaji aliyoyaelezea ni kilimo cha kisasa katika maeneo ya Jiji (urban agriculture) na uwekezaji katika maeneo ya Ranchi.

Timu ya kimkakati ya kutafuta masoko ya miradi ya uwekezaji ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ipo katika ziara ya kutafuta wawekezaji Jijini Dar es Salaam kwa wiki nzima.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.