• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji, TRC kurejesha maisha kwa waliopitiwa na SGR

Imewekwa tarehe: December 30th, 2020

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma kwa kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania katika kutekeleza mpango wa urejeshaji Maisha kwa wananchi waliopitiwa na mradi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Makutopora ili kuwaneemesha wananchi hao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya jana katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya kikao cha wataalam wa taasisi hizo mbili wakati wakati wa utambulisho wa mradi huo.

Nabalang’anya alisema “kwanza niwapongeze TRC kwa mradi huu, ni mradi muhimu sana, naweza kusema kuwa ulipaswa kuanza kabla ya utekelezaji wa fidia. Kwa sasa fidia imeshatolewa kwa wananchi na madhara yake yameshaonekana kwa wananchi kutumia fedha kinyume na matarajio ya mradi na serikali kwa ujumla”.

Alisema kuwa, kama mwananchi alikuwa anamiliki mali kama nyumba au ardhi na baadae mali hiyo ikatwaliwa na akalipwa fidia ili akafanye kile ambacho kilifanyika mwanzo maana yake badala ya kuendelea alirudi nyuma. Alisema kuwa bado nafasi ipo ya kuwaendeleza wananchi hao, “Hatujachelewa, tulipoanzia tuanze kwa vitendo. Kikubwa TRC wamezungumzia program ya mafunzo ambayo ni jambo la msingi sana, hasa mafunzo ya ujasiriamali. Hivyo, tunatakiwa kutambua mahitaji ya mafunzo yanayohitajika kwa jamii, kuwajengea uwezo na kuwafundisha kutasaidia kuwarejeshea maisha” alisema Nabalang’anya.

Mkuu huyo wa Idara aliongeza kuwa baada ya Dodoma kuwa makao makuu, imekuwa na fursa nyingi za kiuchumi. “Dodoma sasa ni makao makuu ya nchi, hivyo mradi wowote ambao utaanzishwa na kusimamiwa vizuri utainua kipato cha mlengwa. Jiji la Dodoma tunaahidi ushirikiano wa kutosha wakati wote katika kufanikisha mpango wa urejesho wa maisha kwa walengwa” alisisitiza Nabalang’anya.

Kwa upande wake msimamizi wa masuala ya kijamii kutoka TRC, Joyce Ponera alisema kuwa kufuatia changamoto zilizojitokeza baada ya kulipa fidia kwa wananchi waathirika wa mradi wa SGR ni matumizi mabaya ya fedha za fidia, TRC imekuja na mpango wa urejesho wa maisha kwa wananchi hao. “Tutawapa mafunzo ya matumizi bora ya fedha yatakayowawezesha kufanya vitu ambavyo vitawaletea maendeleo” alisema Ponera.

Mbali na mafunzo ya usimamizi wa fedha, mafunzo juu ya matayarisho ya ardhi, upataji wa ardhi na ujasiriamali, aliongeza. “Mafunzo haya tutafanya kwa waathirika wa mradi pekee. Aidha, taasisi tutazoshirikiana nazo ni TASAF, SIDO, VETA na mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyo katika mnyororo huo”, alisema Ponera.

Shirika la Reli Tanzania lilifanya kikao kwa ajili ya kuwajengea uwezo wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhusu mpango wa urejeshaji maisha kwa wananchi waathirika wa mradi wa reli ya kisasa SGR.

Wataalam kutoka TRC na Jiji la Dodoma walipokutana kujadili utekelezaji wa mpango wa urejeshaji maisha kwa wananchi waliopitiwa na mradi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Makutopora.

Msimamizi wa masuala ya kijamii kutoka TRC, Joyce Ponera alipokuwa akiongea kwenye kikao na wataalam wa Jiji la Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.