• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tufanye usafi kuepuka magonjwa ya mlipuko - Waziri Dkt. Mollel

Imewekwa tarehe: February 10th, 2022

Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Dkt. Godwin Mollel ametoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika usafi wa mazingira katika maeneo yao ili kuepukana na magonjwa yanayotokana na uchafu.

Mollel ametoa wito huo leo Februari 10, 2022 wakati akizungumza na wafanyabiashara na wananchi katika soko la Mavunde lililopo Kata ya Chang’ombe jijini Dodoma wakati wa zoezi la usafi wa mazingira.

Dkt. Mollel amesema kuwa uchafu wa mazingira katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya biashara na makazi yanasababisha magonjwa ya mlipuko ambayo endapo mwananchi ataugua atalazimika kutafuta matibabu na hivyo kuharibu bajeti ya familia na uchumi wao.

“Mkifanya mazingira yenu kuwa mazuri gharama ya kusafisha mazingira yenu ni kidogo kuliko gharama mtakazotumia kwenda kujitibu magonjwa yanayotokana na uchafu wa mazingira.

“Mojawapo ya vitu ambavyo vitatuongezea uhai ni kufanya usafi, uchafu unapunguza umri wa kuishi kwa sababu watu wengi wanakufa mapema kwa sababu wanaugua magongwa yatokanayo na uchafu hivyo ni muhimu sote tufanye usafi,” alitahadharisha.

Aidha, Naibu Waziri huyo alisema ipo haja kwa Sheria ndogo za Jiji la Dodoma kuwabana wananchi katika usafi wa mazingira pamoja na upandaji wa miti kama wanavyofanya kwenye kuezeka mabati ya rangi katika nyumba zao.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga alisema kuwa kampeni ya kupanda miti inakwenda sambamba na usafi wa mazingira nchi nzima.

Alisema zoezi la usafi lililofanyika leo ni mwendelezo wa shughuli zilizopangwa katika wiki ya uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021 itakayozinduliwa Februari 12, 2022 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango.

Pia Bi. Maganga amewapongeza na kuwashukuru wadau mbalimbali wa mazingira walioshiriki na wanaoendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za mazingira zinazoendelea jijini Dodoma kuelekea uzinduzi huo.

Chanzo: Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira)

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.