• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tumeona mambo mazuri kwa vijana Jiji la Dodoma - UVCCM (M)

Imewekwa tarehe: March 14th, 2020

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dodoma umeipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa utekelezaji wa takwa la kisheria la kutenga asilimia nne kwa ajili ya mikopo ya vijana kutoka katika mapato ya ndani.

Pongezi hizo zimetolewa leo tarehe 14 Machi, 2020 na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Dodoma, Billy Chidabwa baada ya kupokea taarifa fupi ya hali ya ukopeshaji mikopo asilimia nne kwa vijana katika ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Chidabwa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa amesema kuwa taarifa iliyowasilishwa ni nzuri inayoonesha dhamira njema ya Halmashauri kwa vijana. “Taarifa tumeona ni nzuri, tumeona mambo mazuri. Fedha zinatolewa kwa vijana kwa wakati na kwa uwiano wa kuridhisha. Pongezi kwa Halmashauri na Mkurugenzi. Tunamfahamu sana anafanya kazi nzuri” amesema Chidabwa.

Aidha, aliwataka vijana wanaonufaika na mikopo hiyo kufanya marejesho kwa wakati. “Hizi pesa ni ‘revolving fund’, ukirejesha unampa fursa na mwingine kukopeshwa na kunufaika nazo. Jukumu letu sisi ni kuwa mawakili wa changamoto katika jamii, amesema Chidabwa.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya mikopo ya asilimia nne kwa vijana kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Dodoma, Sharifa Nabalang’anya amesema kuwa Halmashauri imeendelea kuongeza wigo wa ukopeshaji vijana. Baada ya kuanza kutekeleza sheria ya kukopesha makundi matatu ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ilikopesha shilingi 2,859,230,000 kati ya fedha hizo shilingi 972,000,000 zilikopeshwa kwa vikundi vya vijana. Idadi ya vikundi vilivyokopeshwa amevitaja kuwa ni 174. “Mwaka wa fedha 2019/2020 tumekopesha awamu moja shilingi 853,000,000. Kati ya fedha hizo shilingi 357,000,000 vilikopeshwa vikundi 40 vya vijana” amesema Nabalang’anya.

Akiongelea changamoto katika ukopeshaji huo, amesema kuwa awali vikundi vya vijana vilivyokuwa vikiwasilisha maombi ya mikopo vilikuwa vichache.  Baada ya kutoa elimu na hamasa kwa jamii, sasa muitikio ni mkubwa na idadi ya maombi ni kubwa kuliko uwezo ameongeza afisa huyo.

Kwa upande wake Katibu wa Hamasa UVCCM Mkoa wa Dodoma, Wilfred Mgomela amesema kuwa ziara hiyo ni ya kimkakati ina lenga kukagua utekelezaji wa asilimia nne ya mikopo ya vijana kama inawafikia vijana. “Katika ziara hii tunakagua vikundi mbalimbali pamoja na utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi”.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Sharifa Nabalang'anya (aliyesimama) akitoa taarifa fupi ya hali ya ukopeshaji mikopo asilimia nne kwa vijana jijini Dodoma kwa wajumbe wa UVCCM Mkoa wa Dodoma katika ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.