• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Tunautaka ubingwa wa FDL" - Kocha Makata

Imewekwa tarehe: July 17th, 2020

Kocha Mkuu wa timu ya soka ya Dodoma Jiji FC inayomilikiwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ameeleza nia yake ya kuchukua ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza nchini baada ya kufanikiwa kupanda ligi kuu kwa kuongoza kwenye kundi B la michuano hiyo.

Kocha Mbwana Makata ameyasema hayo leo kwenye mahojiano mbele ya waandishi wa habari ikiwa ni sehemu ya matayarisho ya mchezo wa kutafuta Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) utakaochezwa kesho saa 10 jioni kwenye dimba la Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam dhidi ya washindi wa Kundi A timu ya Gwambina FC ya jijini Mwanza.

Makata, kocha ambaye amejitengenezea wasifu mkubwa katika soka la Tanzania katika miaka ya karibuni, amefanikiwa kuziongoza timu tatu tofauti kwa misimu mitatu mfululizo kutoka ligi Daraja la Kwanza na kufanikiwa kuzipandisha kuingia Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akiuelezea mchezo wa kesho, Makata amesema wanataraji mchezo utakuwa mgumu kwa kuwa Gwambina ni timu nzuri na imefanya vizuri katika kundi lao, "Tunawaheshimu Gwambina, wana timu nzuri, lakini tuna timu nzuri ya ushindani na tumekuja kuwaonesha kuwa sisi ni wazuri zaidi," amesema Makata.

Naye nahodha wa timu ya Dodoma Jiji FC Mbwana Kibacha amesema "wachezaji wote wako tayari kwa mpambano wa kesho, na wana morari ya juu kuhakikisha wanashinda mchezo huo ili kubeba ubingwa na kuwapa mashabiki wao furaha". Kibacha ameongeza kuwa wamejiandaa vya kutosha na wanataka kudhihirisha uwezo wao kwa kucheza soka safi na la ushindani. 

"Tulifika salama na tumefanya mazoezi ya kutosha kujiweka sawa na mchezo huo, benchi la ufundi chini ya kocha mkuu wamefanya kazi yao, na sisi tuna deni la kutekeleza kile ambacho tumefundishwa ili kupata ushindi" aliongeza Kibacha.

Kocha Mkuu wa Dodoma Jiji FC alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuelekea mchezo wao wa fainali ya ligi daraja la kwanza dhidi ya Gwambina FC.

Nahodha wa timu ya Dodoma Jiji FC Mbwana Kibacha akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maandalizi na mikakati yao kwa mchezo wao wa kesho dhidi ya Gwambina FC ya jijini Mwanza.

Taarifa zilizotufikia katika meza yetu ya habari zinaeleza kuwa tayari viongozi na wapenzi wa Dodoma Jiji FC wameshaanza kuwasili jijini Dar es Salaam kutokea Jijini Dodoma na wengine wataingia kesho ili kuipa hamasa na kuishangilia timu yao. 

Kila la heri Dodoma Jiji FC katika mchezo wa fainali ya ligi daraja la kwanza ngazi ya taifa hapa nchini.  

 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.