• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tushiriki Sensa kwa maendeleo yetu - DC Shekimweri

Imewekwa tarehe: July 23rd, 2022

WANANCHI wa Wilaya ya Dodoma wametakiwa kuitikia rai ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi ili wawe sehemu ya kurahisisha mchakato wa maendeleo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi na wafanyabiashara wa Kata ya Majengo waliojitokeza kwa wingi baada ya kushiriki zoezi la usafi wa mazingira.

Shekimweri alisema “ninawapongeza nyote kwa kujitokeza kwa wingi kufanya usafi. Leo ni tarehe 23 mwezi Julai, siku 30 kamili itakuwa tarehe 23 Agosti, ni siku ya Sensa ya Watu na Makazi. Nataka kuwaomba kuitikia rai aliyoitoa Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwamba kila mmoja ahamasike na kuhamasisha mwingine kuhesabiwa. Tuweze kufahamu Tanzania kuna watu wangapi, wana hali gani za maisha na tena kwa mara ya kwanza mama huyu shupavu anafanya tu siyo Sensa ya Watu lakini pia anahesabu makazi”.

Alisema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza zoezi la Sensa ya Watu na Makazi lifanyike kwa ufanisi na haraka kwa kujaza madodoso kupitia vishikwambi.

Akiongelea umuhimu wa zoezi hilo mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa litasaidia kuleta maendeleo. “Sensa hii itasaidia kwenye kutafsiri mahitaji ya kisera na mipango ya maendeleo na mgawanyo wa fedha za serikali kwa kuakisi hali halisi ya mahitaji ya wananchi” alisema Shekimweri.

Akiongelea utofauti wa Wilaya ya Dodoma na maeneo mengine, alisema kuwa imenufaika sana na bajeti ya serikali. “Sisi wana Dodoma tuna kila sababu ya kujitokeza kwa wingi zaidi kwa kuwa serikali ya awamu ya sita imefanya mambo mengi makubwa ya kupaisha mkoa wetu na wilaya yetu. Sisi ni wanufaika wakubwa sana wa bajeti ya kiserikali. Lakini bado yapo maeneo yenye changamoto, inawezekana takwimu za huku nyuma hazikuwa na uhalisia wa watu walivyo, tujitokeze ili baadae tusilaumu mbona sisi tuna watu wengi lakini hakuna zahanati, tuna watu wengi lakini shule hazitoshi. Inawezekana kuna watu wengi, lakini kwenye Sensa hawakujitokeza kwa hiyo takwimu zilizopo ni za watu wachache” alisisitiza Shekimweri.

Shekimweri ambae ni Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa ya Watu na Makazi Wilaya ya Dodoma aliyataka makundi yote kushiriki kikamilifu. ”Ni muhimu sana makundi yote kwenye kaya zetu na familia zetu kujitokeza kuhesabiwa. Tusinyanyapae na kuwaficha watu wenye ulemavu. Kuna haja ya kufahamu wenzetu wenye ulemavu ni wangapi ili mipango ya serikali iweze kuwafikia” alisisitiza Shekimweri.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.