• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tutoe elimu fasaha, kujikinga na Korona - Shekimweri

Imewekwa tarehe: July 17th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WADAU wa mapambano dhidi ya UVIKO-19 jijini Dodoma wameshauriwa kutoa elimu fasaha ya kujikinga na ugonjwa huo ili kuhakikisha afya za wananchi zinalindwa.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Afya ya Msingi ya Wilaya ya Dodoma mjini, Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea na wajumbe wa kamati hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma leo.

Shekimweri amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendelea na mapambano ya wimbi la tatu la ugonjwa wa UVIKO-19. “Sisi Wilaya ya Dodoma, tunahitaji kupeana elimu sahihi ya kinga ya UVIKO-19 kwa kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa maji tiririka safi na sabuni. Tunatakiwa kuwaambia wananchi ukweli kuwa aina na jinsi ya kuvaa barakoa na inatakiwa ivaliwaje na kwa muda gani” alisisitiza Shekimweri.

Shekimweri ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini alisema kuwa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19 yanaongozwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. “Mapambano haya sio ya mtu mmoja, bali ni yetu sote. Tunataka baada ya kikao hiki tutoke na mkakati jumuishi wa mapambano dhidi ya UVIKO-19 katika wilaya ya Dodoma mjini” amesema Shekimweri.

Akiwasilisha taarifa ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method amesema kuwa UVIKO-19 ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Korona. “Virusi hivi vya Korona ni virusi vipya, tofauti na virusi vingine vya jamii hiyo vilivyowahi kusababisha mlipuko wa magonjwa kama ‘SARS-CoV’ mwaka 2003 na MERS-CoV corona mwaka 2013” amesema Dkt. Method.

Akiongelea wimbi la tatu la maambukizi ya UVIKO-19, Mganga Mkuu huyo amesema kuwa halmashauri imekuwa mstari wa mbele katika kupambana na wimbi la tatu la UVIKO-19. Akiyataja mapambano hayo, ameyataja kuwa ni kupokea na kusimamia miongozo mbalimbali inayoelekeza mapambano dhidi ya ugonjwa huo. “Kusimamia uvaaji wa barakoa kwa watu wote na kusimamia utumiaji wa vitakasa mikono. Nyingine ni kusimamia unawaji wa mikono kwa maji safi tiririka na sabuni” amesema Dkt. Method.

Halmashauri imekuwa mstari wa mbele katika kuelimisha jamii kwa kutumia redio na kuelimisha jamii katika taasisi mbalimbali pamoja na vikundi vya bodaboda, nyumba za ibada, masoko, stendi za mabasi na daladala” ameongeza Mganga Mkuu.

Halmashauri imeshiriki kusambaza na kubandika mabango sehemu mbalimbali zenye jumbe za kujikinga na UVIKO-19. “Taasisi mbalimbali kama shule zimepewa elimu ya afya kuhusiana na UVIKO-19 na kusisitizwa kufuata mwongozo uliotolewa na wizara ya afya wa kujikinga na ugonjwa huo” ameongeza Dkt. Method.

Wilaya ya Dodoma mjini ilipata maambukizi ya UVIKO-19 wimbi la kwanza mwezi Machi mpaka Julai, 2020.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.