• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Tunakwenda kupambana Ligi Kuu" - Dodoma Jiji FC

Imewekwa tarehe: July 19th, 2020

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kudhihirisha ubora wake kuwa siyo kwenye kukusanya mapato ghafi tu bali hata katika mchezo wa soka ambapo timu yake ya Dodoma Jiji FC imetwaa ubingwa wa ligi daraja la kwanza kwa msimu huu wa 2019/2020.

Hayo yamedhihirika baada ya timu hiyo kufanya vizuri katika Ligi ya Daraja la Kwanza kwa kuongoza kundi A na kupanda Daraja kuingia Ligi Kuu Tanzania Bara, huku kubwa likiwa kubeba ubingwa wa ligi hiyo baada ya kuifunga kinara wa kundi B timu ya Gwambina FC ya Misungwi Mwanza goli 1-0 na kutawazwa mabingwa.

Aidha, timu hiyo imezoa zawadi ya kocha bora wa msimu ambaye ni Mbwana Makata na mfungaji bora ambaye ni mshambuliaji wake Anuary Jabir. 

Akizungumza baada ya mchezo wa kumsaka bingwa wa ligi hiyo uliofanyika katika uwanja wa Chamazi Jijini Dar es salaam kocha mkuu wa timu ya Dodoma Jiji Mbwana Makata amewapongeza wachezaji wa timu yake kwa kupambana kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa ligi lakini zaidi kwa kushinda taji la bingwa wa jumla wa michuano hiyo.

Makata alisema kuwa licha ya changamoto nyingi walizokutana nazo na ugumu wa kundi A, lakini wachezaji walionesha kujiamini na kusikiliza maelekezo aliyokua anayatoa kitu kilichopelekea ushindi na kuongeza kuwa, lengo lao sasa lipo kwenye Ligi Kuu huku akiwatoa hofu mashabiki kuwa watafanya vizuri.

“Niwashukuru Bodi ya Ligi kwa kuendesha ligi vizuri, nimshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi, wakuu wa idara na wafanyakazi wote wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma waliojitoa kwa ajili ya timu, wadau wa michezo pamoja na mashabiki wetu kwasababu bila wao tusingekabidhiwa kombe leo, niwaahidi kuwa tunakwenda kupambana na kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu” Aliongeza Makata.

Kwa upande wake msemaji wa timu hiyo Ramadhani Juma amewashukuru Azam Media Group kwa kuonesha mchezo wa fainali hizo mubashara kwani kumewafanya watu kuona ubora wa timu ya Dodoma Jiji na kuondoa makandokando yaliyokuwa yanasemwa kuwa timu hiyo ilikua ikibebwa.

“Kila kitu kilikua wazi kabisa, maneno yalikuwa mengi kuwa tunabebwa, lakini baada ya mchezo wa fainali simu zilikua nyingi kutoka kwa watazamaji kuwa timu yetu imesakata kabumbu safi, na niwahakikishie wana Dodoma kuwa tuna timu nzuri sana kwani tuliwazidi Gwambina kwa kila kitu, tulikua na uwezo wa kufunga zaidi ya goli tatu lakini ndiyo mchezo wa soka ulivyo, hivyo tukutane Ligi Kuu, mazuri yanakuja” alisema Ramadhani.

Naye mfungaji wa goli la ushindi la Dodoma Jiji FC ambaye ndiye kinara wa magoli wa ligi hiyo Anuary Jabir alisema kuwa bado ana deni kwa mashabiki wa timu hiyo la kufanya vizuri katika michuano mikubwa ya Ligi Kuu, huku akimshukuru mwalimu wake, benchi la ufundi pamoja na wachezaji wenzake kwa ushirikiano waliompa hadi akafanikiwa kuwa mfungaji bora kwa kuweka wavuni mabao 11 katika msimu mzima.

Kikosi cha timu ya Dodoma Jiji FC kilichofanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza 2019/20 baada ya kuifunga timu ya Gwambina FC goli 1 - 0 kwenye mchezo wa fainali uliochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi Jijini Dar es Salaam.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.