• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

UJENZI NYUMBA YA WALIMU SEKONDARI MTEMI CHILOLOMA UMEFIKIA VIWANGO

Imewekwa tarehe: December 2nd, 2023

Na. Theresia Nkwanga, HOMBOLO MAKULU

KAMATI ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma imeridhishwa na viwango vya ujenzi wa nyumba ya walimu ‘two in one’ katika Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma na kusema kuwa utakuwa imejengwa kwa viwango bora.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Pili Mbaga alipoongoza Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mbaga alisema kuwa Kamati ya Siasa Mkoa wa Dodoma imeridhishwa na ujenzi wa nyumba ya walimu shuleni hapo. “Mradi wa ujenzi wa nyumba ya walimu ni mzuri na umejengwa na kusimamiwa vizuri. Huko zamani wahandisi walikuwa nyuma katika kusimamia miradi ya ujenzi, lakini siku hizi wapo mstari wa mbele na wanafika katika kusimamia miradi ya ujenzi. Jukumu letu ni kuwaambia wananchi kazi nzuri inayofanywa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hapa tumeambiwa zilitolewa shilingi 95,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya walimu ‘two in one’ na sasa zimeletwa shilingi 216,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha tano na sita” alisema Mbaga.

Akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa nyumba ya walimu kwa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma, Mwl. Livinus Tangayika alisema kuwa serikali kupitia mradi wa kuboresha shule za sekondari (SEQUIP) ilitoa jumla ya shilingi 95,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya walimu ambapo lilikuwa ni hitaji kubwa kwa sababu eneo la shule liko mbali na eneo la makazi ya watu. Fedha za ujenzi ziliingizwa katika akaunti ya shule tarehe 20/6/2023 na kuvuka mwaka na kuanza kutumika katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Akiongelea utekelezaji wa mradi huo alisema kuwa ulianza tarehe 9 Septemba, 2023 baada ya taratibu za manunuzi kukamilika na ujenzi unatekelezwa kupitia ‘force account’. “Mradi huu unahusisha ujenzi wa nyumba moja ya walimu (two in one) yenye vyumba vitatu, sebule, jiko na stoo kwa kila nyumba. Utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 99 ikiwa bado milango michache ambayo ipo kwa fundi katika hatua ya umaliziaji pamoja na ufungaji wa vyoo viwili vya kukaa. Mradi unategemea kukamilika kabla au ifikapo tarehe 25 Novemba, 2023 tayari kwa matumizi” alisema Mwl. Tanganyika.

Kuhusu faida za mradi ukikamilika, alizitaja kuwa ni walimu kukaa kwenye mazingira ya shule na hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji kazi. Nyingine ni kuwezesha mazingira mazuri ya kuishi kwa walimu, aliongeza.

“Uongozi wa Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma unapenda kutoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha hizi ambazo zinaenda kuboresha maisha ya walimu. Pia tunatoa shukrani kwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya, Kamati ya Siasa ya Wilaya kwa maelekezo na usimamizi wa karibu wa miradi yote inayotekelezwa katika Jiji la Dodoma. Hii yote ni katika kuhakikisha kwamba Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inatekelezwa kwa vitendo” alisema Mwl. Tanganyika.

Ikumbukwe kuwa ujenzi wa Shule ya Shule ya Sekondari Mtemi Chiloloma umetumia kiasi cha shilingi 94,823,000 hadi wakati Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dodoma inaitembelea.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.