• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ujenzi wa madarasa uambatane na upandaji miti - Kamati ya Fedha

Imewekwa tarehe: July 17th, 2019

Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeridhishwa na hali ya ujenzi inayoendelea katika shule ya msingi Mnyakongo iliyopo kata ya Nkuhungu jijini hapa.

Kauli hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe baada ya kuongoza kamati ya fedha na utawala kutembelea na kukagua vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi Mnyakongo jana.

Akiongea na wajumbe wa kamati ya fedha na utawala na wajumbe wa kamati ya ujenzi ya shule hiyo, Mstahiki Meya alisema kuwa kazi ya ujenzi iliyofanywa katika shule hiyo ni nzuri. “Nawapongeza wanaosimamia ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule hii. Kazi iliyofanywa hapa ni nzuri. Katika madarasa haya wekeni picha mbalimbali na ramani ili madarasa yawe yanaongea” alisema Prof. Mwamfupe. Aliitaka menejimenti ya Halmashauri kuangalia utaratibu wa kuwapongeza watumishi waliosimamia mradi wa ujenzi wa shule na utunzaji wa fedha katika mradi huo kutokana na kazi kubwa na nzuri waliyofanya. Alipongeza uzalendo unaofanywa na watumishi hao kwa lengo la kuhakikisha miradi hiyo itatekelezwa vizuri kwa mujibu wa mipango iliyopo.

Aidha, aliishauri shule hiyo kupanda miti kuzunguka eneo lote la shule. “Shule hii haina miti, miti inatakiwa kupandwa katika maeneo ya shule ili kutunza mazingira na kupendezesha shule” alisema Prof. Mwamfupe.

Akielezea hali ya utekelezaji wa mradi huo, Mchumi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Happiness Matonya alisema kuwa Halmashauri hiyo ilipeleka tofali 5,100 zilizotolewa na Waziri mkuu shuleni hapo kwa ajili ya ujenzi. Kiasi cha shilingi 15,000,000 zilitolewa na Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kutoka mapato ya ndani kwa aili ya ujenzi wa shule hiyo. Mchumi, aliendelea kufafanua kuwa mpango wa Halmashauri ni kukamilisha madarasa yanayoendelea kujengwa na kuanza ujenzi wa madarasa mengine manne. “Mstahiki Meya, katika bajeti ya mwaka 2019/2020 Halmashauri ya Jiji imetenga shilingi milioni 200 katika bajeti yake kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo, ofisi, umeme na maji” alisema Matonya.

Kwa upande wake, mjumbe wa kamati hiyo, Mhe. Paskazia Mayala alisema kuwa katika mipango ya ujenzi wa shule hiyo suala la viwanja kwa ajili ya michezo ya wanafunzi lizingatiwe. “Mstahiki Meya, viwanja vya michezo vipewe kipaumbele kwa sababu michezo ni muhimu kwa afya za wanafunzi na pia ni sehemu ya masomo yao” alisema Mayala.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha na Uongozi wakiwa na wataalam wa Jiji la Dodoma, kamati hiyo ilipofanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo ya Jiji la Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.