• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ujenzi wa ofisi za Serikali, awamu ya pili yazinduliwa

Imewekwa tarehe: December 2nd, 2021

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua wa awamu ya pili ya ujenzi wa Ofisi za Wizara katika Mji wa Serikali uliopo eneo la Mtumba jijini Dodoma na ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango ihakikishe kuwa fedha kwa ajili ya mradi huo zinapatikana kwa wakati na kikamilifu.

Mheshimiwa Majaliwa ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Desemba 2, 2021) baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora ikiwa ishara ya uzinduzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa Ofisi za Wizara katika Mji wa Serikali.

Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kumpongeza na kumshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha shilingi bilioni 300 ili zitumike katika ujenzi wa Ofisi za Wizara na miundombinu mbalimbali itakayojengwa katika Mji wa Serikali na Jiji la Dodoma.

Mheshimiwa Majaliwa amesema kwamba awamu ya kwanza ya ujenzi wa ofisi 23 za Serikali ulianza tarehe 28 Novemba, 2018 na kukamilika tarehe 22 Machi, 2019 ambapo Shilingi bilioni 39.387 zilitumika kwa ajili ya awamu ya kwanza ya ujenzi huo.

“Watumishi zaidi ya 18,300 wa Serikali Kuu, Bunge, Vyombo vya Ulinzi na Usalama na baadhi ya Taasisi wamehamia Dodoma ambapo kiasi cha shilingi bilioni 162.123 kimetumika kwa ajili ya gharama za posho za uhamisho, ununuzi na usafirishaji wa vifaa, ukarabati na ujenzi wa miundombinu wezeshi ya ofisi.”

Uzinduzi wa huo wa awamu ya pili ya ujenzi wa Ofisi za Wizara na miundombinu mbalimbali zinazojengwa katika Mji wa Serikali ni miongoni mwa matukio ya maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Dar es Salaam Desemba 9, 2021.

Amesema uzinduzi huo ambao utahusisha majengo 24 ya ghorofa unalengo la kuwa na Mji wa Serikali wa kisasa utakaozingatia dhana ya Mji wa Kijani na mji rafiki ili kudhibiti gharama za kiuendeshaji za Serikali za majengo hayo ikiwemo kuzingatia matumizi ya nishati mbadala.

“Awamu ya pili ya ujenzi wa ofisi za Wizara itakwenda sambamba na ujenzi wa miundombinu muhimu ya kudumu ya maji, umeme, mawasiliano, usalama, gesi, TEHAMA, zimamoto na uokoaji, programu za upandaji miti pamoja na ujenzi wa huduma mbalimbali za kijamii.”

“Katika utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais Samia la kuzitaka Wizara kuanza ujenzi mara moja, ninafurahi na kufarijika kuona kwamba tayari Wizara zote zimeshakamilisha taratibu za manunuzi za kuwapata wakandarasi na washauri elekezi wa ujenzi.”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.