• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Reli ya kisasa kupunguza gharama za ujenzi Dodoma

Imewekwa tarehe: February 12th, 2019

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge amesema mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma utakapokamilika utarahisisha usafirishaji wa vifaa vya ujenzi na kuwezesha gharama za ujenzi kupungua Mkoani humo.

Ametoa kauli hiyo alipokuwa akiukaribisha ujumbe wa wageni nane kutoka Jiji la Linz la nchini Austria mjini hapa leo Februari 12, 2018, ukiongozwa na Meya wa Jiji hilo la Linz.

“Reli hii ya kisasa itakapokamilika itarahisisha usafirishaji wa vifaa vya ujenzi na kuwezesha gharama za ujenzi kupungua” alisema Mhe. Dkt.Mahenge.

Dkt. Mahenge alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. John Magufuli imefanikisha dhamira ya kuhamishia Serikali mjini Dodoma na kuufanya Mji huo kuwa Makao Makuu ya Nchi kwa vitendo.

“Dhamira hii ilianzishwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere Mwaka 1973 na imetekelezwa na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. Magufuli” alisema Mhe. Dkt. Mahenge.

Alisema, katika utekelezaji wa dhamira hiyo, Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi, ikiwemo reli ya kisasa ya kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma ambayo baadaye ujenzi wake utaendelea hadi mkoani Mwanza, na kwamba kukamilika kwa mradi huo kutarahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo.

Mheshimiwa Dkt. Mahenge aliueleza ujumbe huo kuwa, Mkoa wa Dodoma una miradi mingi ya ujenzi kutokana na Serikali kuhamia, ikiwemo miradi ya ujenzi wa Ofisi mbalimbali na nyumba za makazi pamoja na miundombinu.

Awali, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Mhe. Prof. Davis Mwamfupe alisema kuwa ziara hiyo ya Mstahiki Meya wa Jiji la Linz inalenga kuendeleza ushirikiano baina ya Jiji lake na jiji la Linz la nchini Austria.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.