• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ushirikishwaji wa wadau nguzo muhimu kufikia malengo ya wadau

Imewekwa tarehe: June 25th, 2024

USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini ni mradi unaofadhiliwa na watu wa Marekani kupitia shirika ya misaada la USAID. Mradi huu unatekelezwa na shirika la Deloitte Consulting kwa kushirikiana na taasisi za kiraia (CSOs) na wadau wengine muhimu katika mikoa kumi na moja nchini Tanzania. Ushirikiano huuunalenga kuimarisha uhusiano kati ya vituo vya afya na jamii, kujenga uwezo, na kutoa huduma bora kwa walengwa.

Mradi unalenga kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, ustawi, na ulinzi kwa Watoto Yatima na Vijana wanaoishi katika mazingira hatarishi (OVC) katika jamii zenye idadi kubwa ya maambukizi ya VVU ndani ya Kanda ya Kusini ya Tanzania. Mradi unalenga kuchangia Malengo ya 95-95-95: kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2030, asilimia 95% ya Watu Wanaoishi na VVU (PLHIV) wanajua hali yao, asilimia 95% ya PLHIV wanaojua hali yao wanapata matibabu, na asilimia 95% ya PLHIV wanaopata matibabu wanapata kufubaza VVU.

Ili kuhakikisha uendelevu na kuendana na vipaumbele vya kitaifa, Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini unafanya kazi kwa karibu na wizara tatu: Wizara ya Afya, TAMISEMI, na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, pamoja na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS). Ushirikiano huu ni muhimu katika kuongeza uwezo wa kusimamia, kuboresha, na kuendeleza upatikanaji wa huduma na mifumo ya kusaidia OVC, na kuendeleza mchango wa mradi katika kudhibiti janga la UKIMWI.


Mnamo Tarehe 21 Juni 2024, wafanyakazi wa mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini walikutana na wadau muhimu wa Serikali mjini Morogoro kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa mradi kwa mwaka wa fedha (FY25) utakaoanza Oktoba mosi 2024 na kukamilika Septenmba 2025. Kikao hiki cha siku mbili kilijumuisha mawasilisho ya mpango kazi uliopendekezwa, ambapo wawakilishi wa serikali walitoa michango na mapendekezo muhimu ili kuhakikisha mipango ya mradi inaendana na vipaumbele vya Serikali na upatikanaji wa huduma bora kwa walengwa.

Baada ya mawasilisho, mjadala mkubwa ulijikita katika maeneno tofauti, ikiwa ni pamoja na uendelevu wa mradi, kujengeaa uwezo wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii, kushirikisha wadau mbalimbali katika ngazi tofauti, kuboresha mfumo wa rufaa kati ya vituo vya kutolea huduma za afya na watoa huduma ngazi ya jamii na kuimarisha mifumo ya serikali. Wawakilishi wa serikali walitoa ushauri muhimu juu ya kuboresha ushirikiano na kuhakikisha uendelevu baada ya mradi kuisha.

Washiriki wa kikao hicho walitembelea maeneo mbalimbali ya mradi, ikiwemo vituo vya afya, kaya, na vikundi vya kuimarisha uchumi. Madhumuni ya ziara hizi ilikuwa ni kuongeza ufahamu zaidi juu ya malengo mahususi ya mradi na namna unavyoboresha maisha ya walengwa.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa wizara kwa ushirikiano wao endelevu. Ushirikiano huu ni muhimu katika nia ya kufikia malengo ya mradi ya kulinda na kuboresha maisha ya Watoto Yatima na Vijana wanaoishi katika mazingira hatarishi katika Kanda ya Kusini ya Tanzania

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.