• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Utekelezaji Ilani safi, kongole DUWASA - CCM Wilaya

Imewekwa tarehe: August 27th, 2021

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Siasa Wilaya ya Dodoma imeridhishwa na utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) unaofanywa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Dodoma (DUWASA) ya kuwasogezea wananchi huduma ya maji.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Dodoma, Meja Mst. Johnick Risasi wakati alipoongoza hiyo kutembelea kituo cha kuzalisha Maji Mzakwe jijini Dodoma.

Meja Mst. Risasi kuwa baada ya kamati ya siasa kutembelea na kukagua kazi inayofanywa na DUWASA imeridhika. “Kamati ya Siasa ya Wilaya imepita kukagua kazi inayofanywa na DUWASA na imejiridhisha na utekelezaji wa miradi ya Maji inayotekelezwa wilayani Dodoma. Nichukue nafasi hii kuwapongeza sana DUWASA kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi” alisema Meja Mst. Risasi kwa uhakika.

Akiongelea uhusiano baina ya upatikanaji wa huduma ya Maji na maendeleo, Mwenyekiti huyo alisema kuwa Maji yanachochea maendeleo. “Ndugu zangu Maji ni uhai, mnatuona tunatakata hapa kwasababu ya Maji. Tuwashukuru sana DUWASA kwa huduma hii nzuri. Bila Maji hatuwezi pata maendeleo. Mtakumbuka kuwa watu walikuwa wanatumia muda mrefu kutafuta huduma ya Maji. Sasa huduma hii inapofikishwa kwa wananchi, wanatumia muda zaidi katika shughuli za maendeleo” alisema Meja Mst. Risasi.

Akitoa maelezo ya hali ya huduma ya maji mjini Dodoma, mwalikishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA, Sebastian Warioba alisema kuwa hali ya usambazaji ni nzuri. “DUWASA imefanikiwa kuunganisha huduma ya majisafi kwa wateja 56,266 kupitia maunganisho haya, DUWASA imeweza kuhudumia asilimia 62.7 ya wakazi” alisema Warioba.

Warioba alisema kuwa DUWASA imefanikiwa kuondoa mgao mkali wa maji uliokuwepo kabla ya kuanzishwa kwa DUWASA mwaka 1998. “DUWASA imefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha huduma ya maji ikiwepo mradi ulioongeza uwezo wa uzalishaji maji Mzakwe kutoka lita milioni 30 kwa siku hadi lita Milioni 61 kwa siku uliokamilika mwaka 2015” alisema Warioba.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Rukia Bakari aliwapongeza DUWASA kwa kazi nzuri ya kusogeza huduma ya maji kwa wananchi. “DUWASA hongereni kwa kazi nzuri. Kweli kazi imefanyika na inaonekana. Huu ni utelekezaji wa Ilani ya CCM ulio wazi. Halmashauri ya Jiji itaendelea kutoa ushirikiano kwa DUWASA ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi zaidi” alisema Bakari.

DUWASA ina mtandao wa majisafi wenye urefu wa Kilometa 687.07.

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Dodoma, Meja Mst. Johnick Risasi (kushoto) akisisitiza jambo kwa mwalikishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA, Sebastian Warioba (kulia) wakati Kamati Siasa Wilaya ilipotembelea miradi inayotekelezwa katika Wilaya ya Dodoma, katikati ni mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Rukia Bakari.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.