• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Uwasilishaji wa Ritani za Kodi sasa Kielektroniki - TRA

Imewekwa tarehe: August 23rd, 2020

Mfumo wa Ritani mtandaoni utawarahisishia wafanyabiashara nchini - TRA

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imezindua mfumo wa uwasilishaji wa taarifa kwa mlipa kodi na kuwataka wafanyabiashara wote wakubwa nchini kutumia ili kuondokana na changamoto mbalimbali zilizokuwa zikijitokeza hapo awali.

Akizungumza jijini Dar es Salaam tarehe 19/08/2020, Kamishna wa Walipakodi Wakubwa TRA, Alfred Mregi, alisema kimsingi ujio wa mfumo huo uliozinduliwa rasmi Agosti 6 Mwaka huu, utawasaidia wafanyabiashara pamoja na TRA kuepuka upotevu wa muda pale mwananchi anapotakiwa kupeleka taarifa fulani zinazohusu kodi.

Mregi alisema awali kabla ya kuzinduliwa kwa mfumo huo wateja wao hao ambao ni walipa kodi wakubwa walikuwa wakilazimika kuwasilisha taarifa hizo kwa njia ya kawaida kwa kupeleka taarifa zao moja kwa moja katika ofisi za TRA tofauti na sasa ambapo mteja ataweza kutuma taarifa akiwa mahali popote.

“Kwa sasa wataweza kuwasilisha taarifa zao kutoka mahali popote, hii mbali na kuokoa muda waliokuwa wakiutumia kwenda katika ofisi zetu, pia mfumo huu utawasaidia wafanyakazi wetu kuondokana na hali ya kukosea kosea katika uingizaji wa taarifa hizo katika mfumo wetu hivyo kuathiri makadirio,” alisema Mrige.

Aidha alisema kupitia mfumo huo mpya, wafanyabiashara wataweza kupata majibu ya moja kwa moja ya mapokeo ya kodi yake ndani ya wakati, tofauti na hapo awali ambapo alilazimika kusubiri taarifa pale ambapo itakuwa imeshapigwa muhuri kutoka TRA.

“Kodi inalipwa kutokana na makadirio tunayoyafanya kwa biashara husika, hivyo unapopata taarifa sahihi ndipo hapo utakapoweza kukadiria ipasavyo kuwa ni kiasi gani unapasa kutoza, kimsingi mfumo huu umekuja kama mkombozi katika shughuli nzima ya ukusanyaji wa mapato kwa wafanyabiashara huku tukiamini kuwa hata wao wataufurahia.

Katika hatua nyingine Kamishna huyo wa walipakodi wakubwa aliwakumbusha waajiri wote nchini kuhakikisha wanawakumbusha wafanyakazi wao kuwapatia namba za mlipakodi (TIN) kwa ajili ya utekelezaji wa masuala mbalimbali yanayohitajika na TRA hususani katika kupata taarifa sahihi za watumishi hao ili iweze kuwa na usahihi katika viwango vya kodi inayopasa kuitoza.

Alisema mfumo huo wa uhitaji wa TIN umelenga kuhakikisha waajiri wanatoa taarifa sahihi tofauti na hapo awali ambapo wengi walikuwa wakidanganya na hivyo kusababisha TRA kupata hasara kutokana na kutoza kodi kwa idadi ndogo ya wafanyakazi tofauti na uhalisia kamili.

Chanzo: HabariLeo


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.