• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Uwekaji anuani makazi washika kasi, mitaa 222 kutambuliwa

Imewekwa tarehe: February 16th, 2022

JUMLA ya mitaa 222 iliyopo ndani ya kata 41 za halmashauri ya Jiji la Dodoma, zinatarajiwa kuwekewa anuani za makazi ili kurahisisha utoaji wa huduma mbalimbali za kimawasiliano, kiusalama, kiuchumi ikiwemo kukusanya kodi mbalimbali kwa urahisi na kurahisisha kazi za uokoaji na kuzuia maafa wakati wa majanga kama ajali ya moto.

 Mratibu wa mfumo wa uwekaji anuani za makazi Jiji la Dodoma Joseph Nkuba alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Jijini humo.

Nkuba alisema kuwa mitaa hiyo itakayowekewa anuani itaongeza ufanisi kwenye mitaa mbalimbali katika kufikisha bidhaa na kuzuia upotevu, na kwa wananchi kurahisisha kutambua makazi yao.

Mratibu huyo alisema zoezi hilo limeshaanza kwa hatua za awali huku akitaja faida zingine za mfumo huo kuwa ni kurahisisha huduma za ulinzi na usalama, kuongeza ufanisi katika usimamizi wa makazi ya watu na kutambua mali na upatikanaji wa takwimu mbalimbali.

Zingine ni kuongeza tija na ufanisi katika huduma za uokoaji na kuzuia maafa, kuwezesha ukusanyaji wa kodi mbalimbali kwa urahisi na kwa wakati ikiwa na pamoja na kupambana na uhalifu katika kupata taarifa za uhamiaji na shughuli za utalii.

“Uwekaji wa anuani za makazi ulianza katika hatua za awali Disemba 13, 2021 kwa kutambua mipaka ya mitaa 153 na hadi sasa iliyobaki ni mitaa 69 na itakamilishwa ifikapo Mei 22 mwaka huu.

“Pia katika kuhakikisha zoezi hilo linakamilika kwa wakati ulioelekezwa na Serikali, Jiji linatarajia kuajiri vijana wasiopungua 100 wenye sifa ikiwemo ya elimu ya kidato cha nne, wataalam wa kutumia kompyuta na wale wenye uwezo wa usomaji wa ramani ambapo watafanya kazi hiyo kwa siku 45” alisema Nkuba.

Aidha, mratibu huyo ametoa tahadhari kwa wananchi kutolihusisha zoezi hilo la uwekaji wa anuani za makazi na upimaji wa viwanja, badala yake wawe na ushirikiano kwa serikali kwenye zoezi hilo ili liweze kukamilika kwa wakati, na kwamba hilo ni zoezi la kitaifa na linafanyika katika kila Halmashauri hapa nchini.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.