• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Uzalendo wahitajika utekelezaji miradi ya serikali

Imewekwa tarehe: October 30th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule leo Oktoba 30, 2023, amehudhuria hafla ya utekelezaji wa Mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya Miji Tanzania ikihusisha ushindani (TACTIC) kwa Mkoa wa Dodoma unaotekelezwa na Kampuni ya CHINA GEO ENGINEERING CORP chini ya Mhandisi Msimamizi HONG - IK CONSULTANT CO. LTD kwa kushirikiana na GAUZE- PRO CONSULT (T) LTD na G & Y ENGINEERING CONSULT PLC hafla ambayo imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mradi huo unaotekelezwa na Serikali kuu chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia, una lengo la kuboresha miundombinu ya Barabara, madaraja, mitaro, majengo mbalimbali, vivuko vya barabara n.k pia una lengo la kujengeana uwezo kwa Taasisi tofauti tofauti.

Akizungumzia wakati wa hafla hiyo, Mhe. Senyamule amesema Dodoma ina hadhi ya Miji ya Kimataifa kutokana na vipimo vya hadhi hiyo hivyo miradi hii izingatie hadhi ya Jiji hili.

"Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ana maono na utashi mkubwa kwa Dodoma hivyo tunataka Jiji la Dodoma kuwa na hadhi ya Kimataifa kwani Mkoa huu umepimwa kwa asilimia 80 lakini tunataka kufikia asilimia 100. Dodoma haifananishwi na majiji mengine bali Miji mikubwa ulimwenguni hivyo, miradi hii ijengwe kwa hadhi hiyo na ubora huo wa Kimataifa. Nataka Mradi huu uwe moja ya miradi tunayopata taarifa yake kila mwezi" Mhe. Senyamule.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri, amesisitiza uzalendo kwa wasimamizi wa mradi huu pia matumizi mazuri ya fedha kwani zinatoka moja kwa moja kutoka Benki ya Dunia.

"Mradi huu si wa Jiji pekee Bali na wadau ambao ni Taasisi za miundombinu. Hatuhitaji ucheleweshwaji wa kukamilika kwake kwani mradi unasimamiwa na Jiji lakini fedha inatoka Benki ya Dunia hivyo kusiwepo na minong'ono ya fulani anakula fedha kwani hakuna ambaye itapita mikononi mwake. Tutangulize uzalendo kwenye hii kazi, tunataka tuone thamani ya fedha na kukamilika kwa mradi kwa wakati" Mhe. Shekimweri

Aidha, Mbunge wa Jiji la Dodoma Mhe. Anthony Mavunde amebainisha kuwa Dodoma ni kati ya mikoa inayoongoza kwa kuwa na mtandao mrefu wa barabara unaofikia takribani Km 70 hivyo miradi hii itasaidia kuliboresha Jiji la Dodoma kwa hadhi yake ya Makao makuu ya nchi. Pia amesema, miradi hii inakwenda kuboresha upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii. Ametoa Rai kwa viongozi kusimamia miradi hii kwa dhati ili wananchi waweze kushuhudia matokeo yake.

Mradi wa TACTIC ulisainiwa mara ya kwanza tarehe 13 Septemba 2023 chini ya Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa ambapo unahusisha ujenzi wa miundombinu kwa awamu tatu ambapo awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa masoko, mitaro, vivuko, stendi za mabasi, n.k na mpaka sasa maeneo yote yatakayojengwa chini ya Mradi huu yameshafanyiwa usanifu na tayari mkandarasi yupo katika hatua ya maandalizi kwa kufikisha vifaa kwenye eneo la ujenzi . Mradi unagharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 24 bila Kodi ya ongezeko la thamani ( VAT) na unatarajiwa kutumia kipindi cha miezi 15

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.