• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Uzinduzi wa Mtandao wa mabomba ya Maji safi - Kinyambwa Extension

Imewekwa tarehe: August 14th, 2019

MWENGE wa Uhuru mwaka 2019 umezindua mradi wa Mtandao wa mabomba ya kusambazia maji safi kwenye mtaa wa Kinyambwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuwahakikishia wananchi uhakika wa maji safi na salama.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Mzee Mkongea Ali baada ya kukagua na kuzindua Mtandao wa mabomba ya kusambazia maji safi eneo la Kinyambwa ’Extension’ wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Dodoma mjini, alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha tatizo la maji linakuwa historia nchini kwa kusogeza huduma hiyo karibu na wananchi. Serikali itaendelea kujenga miundombinu ya maji ili kuboresha upatikanaji wa maji.

Awali akiwasilisha taarifa ya mradi wa ujenzi wa mtandao wa mabomba ya kusambazia maji safi eneo la Kinyambwa ’Extension’, Mhandisi David Pallangyo alisema kuwa mradi huo wenye mabomba yenye urefu wa kilometa 5.34 umetekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira mjini Dodoma (DUWASA). “Lengo kuu la mradi huu ni kufikisha huduma ya majisafi kwa wakazi wa eneo la Kinyambwa Extension, huduma ambayo itachochea shughuli za kijamii, ujenzi na uendelezwaji wa viwanja ambavyo tayari vimegawiwa kwa wananchi. Mabomba yaliyolazwa ni ya plastiki yenye vipenyo vya kati ya  inchi 2 na  inchi 6, alisema Mhandisi Palangyo.

Akiongelea utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi huyo alisema kuwa sehemu kubwa ya kazi ya ujenzi wa mtandao wa mabomba ya kusambazia maji eneo hilo ilifanywa na mamlaka yake kwa gharama ya shilingi 103,893,668. “Sehemu ndogo ya kazi ya kuchimba na kufukia mtaro, ujenzi wa chemba na ujenzi wa alama za njia ya bomba imefanywa na Mkandarasi Kampuni ya M/S. BAHAJ Construction Works. Kazi za ujenzi wa mtandao wa mabomba eneo hili ilianza 23/03/2019 na kukamilika 31/05/2019” alisema Mhandisi Palangyo.

Mradi huo umekamilika, na wateja 17 wameunganishiwa huduma ya maji wakati maombi 29 yamepokelewa kwa ajili ya kuunganishiwa huduma hiyo. Aidha, viwanja 1,743 vinatarajiwa kuunganishwa na huduma ya majisafi katika eneo hili, ambavyo ni sawa na jumla ya watu wapatao 10,458.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.