• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Vijana Tanzania walioamua kubadili mtizamo wa kazi ya uchuuzi wa mitaani

Imewekwa tarehe: March 18th, 2020

Ni Jambo la kawaida, unapokuwa unatembea mitaani katika nchi za Afrika kukutana na wachuuzi wa mtaani al maarufu wamachinga, kutokana na ukosefu wa ajira, lakini Alexanda Manyika na Noah Jotum ni wamachinga wanaobadili mtizamo wa kawaida kuhusu wachuuzi hao.

Mara nyingi, muonekano wa vijana hawa unakuwa sio wa kupendeza sana wala kuvutia kutokana na mavazi yao, hivyo kutowavutia wateja.

Ili kukabiliana na changamoto hiyo, baadhi wa wachuuzi wameanza kuona umuhimu wa kazi yao hivyo kubuni njia mbalimbali za kuvutia wateja, ikiwemo kuvaa vizuri na kuwa watanashati.

Miongoni mwao, ni Alexanda Manyika na Noah Jotum ambao wote ni wachuuzi kutoka Mkoani Dodoma, nchini Tanzania, hawa ni vijana ambao wamekuwa wakiuza manukato mitaani kwa takriban miaka mitano sasa.

Mwanzo ukiwaona utadhani ni mapacha, vimo vyao vinafanana lakini zaidi pia unaweza kuwaweka katika kundi la wasanii chipukizi kutokana na mavazi yao ya kufanana. Wamejijengea umaarufu kutokana na utanashati wao ambao umekuwa ni gumzo mitaani.

"Unajua biashara ni ubunifu," Alexanda aliiambia BBC jijini Dodoma huku akiwa amebeba mfuko wake wa manukato na kujawa na bashaha. "Na lengo la kuvaa hivi ni sehemu ya ubunifu wetu. Huu umekuwa ni utambulisho na imetufanya tuwe tofauti na wengine. Ni kutokana na mavazi yetu mtu anaweza kusimamisha gari na kuuliza kuna nini," aliongeza.

Alexandar ndiye mwanzilishi wa ubunifu huo na baadae aliamua kupanua wigo kwa kumwingiza Noah katika biashara hiyo, na hivi sasa wanafanya kazi kama washirika.

Noah ana umri wa miaka mitatu tangu aingie katika biashara hiyo na anasema watu wanavutiwa sana na mtindo wao wa mavazi. "Kwa jinsi tunavyovaa, watu wanavutiwa sana na sisi, na hivyo kuongeza mapato, pia wateja wameanza kutuamini kwa muonekano wetu mbele ya watu," anasema Noah.

Je kuna uwiano wowote kati ya mavazi na faida wanayoipata? Alexanda anasema bei ya mavazi yao sio ya kutisha, bali ni bei za kawaida, ila kinachofanyika kikubwa ni ubunifu.

"Naweza kuchukua koti la kawaida, nikaliongezea ubunifu hapa na pale, na baadae likatoka tofauti kabisa. Sio gharama. Tunafahamu ili tuendelee lazima tujibane kwenye matumizi, na haya mavazi hayatuumizi," anasema Alexanda.

Vijana wengi ambao hawana ajira aidha wameshindwa kuona fursa ya kujiajiri kupitia umachinga au wamekuwa wakidharau kazi hii kwa kuhisi kipato chake ni kidogo. Hata hivyo, Alexanda na Noah ni miongoni mwa vijana wanaojivunia kwa mafanikio waliyoyapata kupitia kazi ya uchuuzi.

"Niseme tu wazi bila kificho. Kazi hii imenisaidia sana. Kwanza mbali na kipato, imenisaidia pia kimawazo, hata kukua pia kifikra, kuongeza ujasiri zaidi, hata kuongea mbele za watu, lakini tukirudi kwenye eneo la uchumi ambalo ndio lengo zaidi, biashara hii imenisaidia kuweza kulipia makazi yangu mwenyewe, lakini pia mavazi, kujilisha, lakini pia nimeweza kusomesha wadogo zangu na kuwasaidia wazazi wangu katika shida zao mbalimbali," anasema Alexanda.

Wateja wanaonekana kuvutiwa na muonekano wa Alexanda na Noah.

Amina Njogolo, ambae ni mteja anasema, "Ninapohudumiwa na watu wa aina hii ambao wapo smati kwanza najisikia vizuri na pia inanipa hali ya kuwaamini tofauti na vijana wengine ambao sio watanashati unaweza kuwadhania pengine waizi."

Nae Abdallah Twaha, anasema katika biasha ubunifu ni muhimu na hasa suala la utanashati kwa sababu wateja wanapenda kuhudumiwa na watu wasafi na wanaovutia.

Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika mashariki zinazokabiliwa na wimbi kubwa la ukosefu wa ajira kwa vijana wanaohitimu katika vyuo mbambali vya elimu ya juu na standi za ufundi. Mpaka sasa mkazo mkubwa umewekwa katika ujasiriamali ambapo ndipo kulipo na fursa za watu kujiajiri.

Chanzo: bbcswahili


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.